RAIS KIKWETE AWAPANDISHA VYEO MAOFISA WA JESHI.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dk. Jakaya Kikwete, amewapandisha cheo maafisa wakuu kutoka Kanali kuwa B...

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Dk. Jakaya Kikwete, amewapandisha cheo maafisa wakuu kutoka Kanali kuwa Brigedia Jenerali.

Taarifa ya Kurugenzi ya Habari na Uhusiano Makao Makuu ya Jeshi, ilieleza jana kuwa Rais amezingatia Kanuni za Majeshi ya Ulinzi, Aya ya 7.01 Kifungu cha 13 Juzuu ya Kwanza (Utawala).

Maafisa Wakuu hao ni Kanali Denis Raphael Janga, Kanali Jason Nestor Musikula, Kanali Jackson King Mrema, Kanali Martin Amos Kemwaga, Kanali Joseph Cosmas Chengelela, Kanali Martin Nikubuka Mwankanye, Kanali Harold Kidundi Mziray, Kanali Emmanuel Peter Kapesa na Kanali Mwita Wambura Isamulyo.

Wengine ni Kanali Francis Asilia Njau, Kanali Pendo Uledi Kamungwele, Kanali Moses Adolph Shinyambala, Kanali Ibrahim Abdarahamani Kimario, Kanali Michael Garo Luwongo, Kanali Nelson Hosea Msanja, Kanali Blasius Kalima Masanja, Kanali Aloyce Damian Mwanjile, Kanali Rajabu Goma Hanti, Kanali Ignas Beatus Mubofu na Kanali Dominic Basil Mrope. 

Pia wamo Kanali Hamis Issa Majumba, Kanali Salehe Omari Semtaua, Kanali Henry Sweko Kamundo, Kanali Sylivester Msafiri Minja, Kanali John Bangantagoka Bishoge, Kanali Anselm Shigongo Bahati, Kanali Robinson Mboli Mwanjela na Kanali Kaisy Philip Njelekela. 

Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), Luteni Jenerali Samueli Ndomba kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange, aliwataka kuendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuleta tija na maendeleo katika JWTZ na Taifa kwa ujumla.

Aidha, Luteni Jenerali Ndomba alisisitiza kusimamia nidhamu na ueledi.

Related

TASWIRA ZA MATUKIO MBALIMBALI KATIKA ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM HUKO TARIME MKOANI MARA

Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kama ishara ya kufungua ofisi ya CCM Tawi la Nyabichune,wilaya ya Tarime mkoani Mara. Katibu Mkuu wa CCM Taifa Ndugu Abdulrahman Kinana ...

Rais wa Zanzibar, Dk Shein afungua jengo jipya la ZAPHA+

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein,akikata utepe kama ishara ya kulizindua jengo jipya la Jumuiya Wanaoishi na Virusi vya Ukimwi ZAPHA+ huko Welezo jana,(k...

YANGA YAKUBALI KIPIGO CHA MABAO 3-2 KUTOKA KWA AZAM

Mshambuliaji wa Yanga Didie Kavumbago akipimana msuli na mliniz wa Azam FC Kipre Balou katika mchezo huo. Mshambuliaji wa Yanga Hamis Kiiza akichuana na mlinzi wa Azam FC, Waziri Salam wakati w...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904821
item