AJINYONGA KWA KUKOSA KODI YA CHUMBA
Marehemu Geofrey Ndibalema (41), mkazi wa Tandika jijini Dar aliyejinyonga kwa kukosa kodi ya chumba INASIKITISHA! Geofrey Ndiba...
https://gabriellabridalsolution.blogspot.com/2014/06/ajinyonga-kwa-kukosa-kodi-ya-chumba.html
Marehemu Geofrey Ndibalema (41), mkazi wa Tandika jijini Dar aliyejinyonga kwa kukosa kodi ya chumba
INASIKITISHA! Geofrey Ndibalema (41), mkazi wa Tandika jijini Dar amedaiwa kujinyonga kwa kukosa kodi ya chumba.
Tukio
hilo la kusikitisha limetokea Juni 14, mwaka huu katika nyumba
aliyopanga marehemu ambapo ilidaiwa kuwa siku moja kabla ya tukio, baba
mwenye nyumba alimpigia simu kumkumbushia akaahidi kulipa siku
iliyofuata ambayo ndiyo alikutwa amejinyonga.
Kwa
mujibu wa ndugu wa karibu wa marehemu aliyeomba hifadhi ya jina lake,
alisema Geofrey aliamka asubuhi akiwa mzima wa afya na kwenda kuchota
maji ya kuoga ili aelekee kwenye shughuli zake za upambaji ambapo
ilidaiwa kuwa alipewa tenda ya kupamba katika harusi na tayari
alishachukua nusu ya malipo..
Marehemu Geofrey Ndibalema (wa pili kulia) enzi za uhai wake.
Ndugu
huyo wa marehemu alidai, wakati Geofrey anarudi kuchota maji, alimkuta
mwenye nyumba akiwa anamsubiri ili alipe kodi yake jambo lililodaiwa
kumpa hofu marehemu na kuingia ndani ya chumba chake na kujinyonga.
“Mwenye
nyumba alibaki anasubiri alipwe kodi kwa kuwa alijua Geofrey aliingia
chumbani kwake kwa ajili ya kuchukua hela hiyo lakini muda mrefu ulipita
bila kutoka nje kiasi cha mwenye nyumba kuanza kupata wasiwasi lakini
aliamua kumuacha na kuondoka,” alisema ndugu huyo.
Ndugu
huyo alizidi kueleza kuwa, baada ya muda rafiki wa marehemu aitwaye
Dickson aliyekuwa akiishi naye chumba kimoja ndiye aliyegundua mwenzake
alikuwa amejinyonga.
“Rafiki
yake aligonga sana mlango bila mafanikio ndipo alikwenda dirishani na
kuendelea kuita bila mafanikio, lakini alipochungulia alimuona Geofrey
akiwa ananing’inia ndipo alipotutaarifu tukaja,” alisema ndugu huyo.
Ndugu
huyo alisema baada ya taratibu za kipolisi kukamilika, walimsafirisha
marehemu mkoani Kagera kwa ajili ya mazishi huku ikielezwa baba mwenye
nyumba na wanakamati wa harusi waliompa tenda marehemu wamesamehe madeni
yao.