TAARIFA RASMI KUTOKA JESHI LA MAGEREZA DHIDI YA UZUSHI KUWA BABU SEYA NA MWANAE WAMEACHIWA HURU

TANGU majira ya mchana kuna taarifa zilizagaa kwamba Babu Seya na mwanae Papi Kocha walikuwa wameachiwa huru na kuanza kusambazwa ujumbe...


TANGU majira ya mchana kuna taarifa zilizagaa kwamba Babu Seya na mwanae Papi Kocha walikuwa wameachiwa huru na kuanza kusambazwa ujumbe mfupi wa simu za mkononi na kwenye mitandao ya kijamii.

Hata hivyo Jeshi la Magereza limefunguka na kuweka bayana juu ya ukweli wa taarifa hizo kama taarifa yao inavyosomeka hapo chini;

Hivi sasa kuna taarifa zimesambaa kupitia Ujumbe mfupi wa simu (SMS) na mitandao ya kijamii zikihusisha kuachiliwa huru kwa wafungwa wawili wanaotumikia Kifungo cha Maisha gerezani. Wafungwa hao wanaotajwa ni Nguza Vicking(Maarufu kwa jina Babu Seya) na Johnson Nguza(Maarufu kwa jina la Papii Kocha).

Napenda kuufahamisha Umma wa Watanzania kuwa taarifa hizo zote zilizotolewa kupitia njia hizo ni za Uongo na uzushi mkubwa na zinalenga kuipotosha jamii kwani wafungwa hao wapo gerezani na wanaendelea kutumikia adhabu ya kifungo cha Maisha gerezani kwa mujibu wa Sheria.

Jeshi la Magereza nchini linatoa onyo kali kwa watu kujiepusha na uhalifu huo na linawataka wale wote wanaotumiwa ujumbe wa aina hiyo waepuke kuusambaza ujumbe huo kwa wengine bali waufute, kwani kuendelea kuusambaza ni kosa kisheria.

Aidha, Jeshi la Magereza linaendelea na uchunguzi wa kina ili kuwabaini wanaosambaza ujumbe huo likishirikiana na Vyombo vingine muhimu kwa lengo la kuwakamata wahalifu hao ili mkondo wa Sheria uchukue nafasi yake.

Imetolewa na;
Lucas Mboje, Mkaguzi wa Magereza,
Afisa Habari wa Jeshi la Magereza,
Makao Makuu ya Jeshi la Magereza,
DAR ES SALAAM.
Septemba 8, 2014

Related

TAZAMA PICHA: NYUMBA ZA JESHI LA POLISI ZILIVYOTEKETEA KWA MOTO TANGA

  Nyumba za Askari wa jeshi la polisi zilizopo eneo la chumbageni nyuma ya kituo kikuu  cha polisi cha chumbani jijini Tanga zaliungua moto.  Mh.Halima Dendegu akishuh...

GODFREY MGIMWA ASHINDA UBUNGE JIMBO LA KALENGA

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Kalenga, Iringa Pudenciana Kisaka amemtangaza Godfrey Mgimwa - CCM kuwa mshindi wa Ubunge kwenye Jimbo hilo. Matokeo ya mwisho ya uchaguzi huo ni kama yanavyoonekan...

TAARIFA YA KATIBU WA BUNGE MAALUM LA KATIBWA KWA VYOMBO VYA HABARI

BUNGE MAALUM  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI  RATIBA YA MKUTANO WA BUNGE MAALUM TAREHE 17 HADI 21 MACHI, 2014  Ofisi ya Katibu wa Bunge Maalum inawatangazia Wajumbe wa Bunge Maal...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904758
item