MWANAFUNZI WA MWAKA WANNE WA SHERIA ALIYEJERUHIWA KWA RISASI USIKU WA KUAMKIA LEO ANAENDELEA VYEMA BAADA YA KUONDOLEWA RISASI MWILINI

Mwanafunzi aliyejeruhiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo amefanyiwa operation na zoezi hilo limemalizika salama na hivi sasa yupo kwenye m...


Mwanafunzi aliyejeruhiwa na majambazi usiku wa kuamkia leo amefanyiwa operation na zoezi hilo limemalizika salama na hivi sasa yupo kwenye moja za wodi za hospitali ya Muhimbili. Taarifa hiyo imetolewa muda si mrefu na mkuu wa chuo kikuu cha Dar es salaam Pro. Mukandara, wakati alipopewa nafasi ya ufunguzi wa mjadala wa kigoda cha Mwalimu unaondelea muda huu kwenye ukumbi wa Nkuruma wa chuo kikuu cha Dar es salaam.

TUJIKUMBUSHE
Usiku wa kuamkia leo wanafunzi wa mwaka wa nne wa chuo kikuu cha mlimani wanaochukua shahada ya sheria
walivamiwa na majambazi maeneo ya Yombo chuoni hapo. Wanafunzi hao walikuwa wanajisomea na kuandaa “Disertation” zao na kujikuta wakivamiwa na watu wanne na kuamuriwa watoe komputa zao na pochi za fedha. Kwa mujibu wa chanzo cha habari hii kutoka chuoni hapo, wanafunzi hao walikubali kuwapa komputa hizo na pochi za fedha,  na majambazi kuanza safari yao.

Baadaye wanafunzi hao wakawaomba wapate hata nakala (Soft Copy) ya vitu vyao, na ndipo mmoja wao akaamua kuwafuata na kukumbana na risasi tumboni. Mwanafunzi huyo baada ya kupigwa risasi alianguka chini na kugaagaa chini huku akikosa msaada wa kupelekwa Hospitalini.

Chanzo kimeendelea kusema kuwa wanafunzi wa Chuo hicho waliwasiliana na uongozi ili kupata gari ili wamkimbize mwenzao Hospitalini, lakini ilipita takribani nusu saa hakuna majibu na ndipo walipoamua kujikusanya na kuamua kuwafuata viongozi. Kwa sasa mwanafunzi huyo amekimbizwa Hospitalini kupata matibabu zaidi.

Tukio hilo limelaaniwa vikali na UMMA wa chuo kikuu cha Dar es salaam na kuitaka serikali kufuatiliwa na kudhibiti vitendo hivyo vya kikatili chuoni hapo. 

Related

UKAWA WATISHIA KUANDAMANA NCHI NZIMA

Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), umemtaka Rais Jakaya Kikwete kusitisha mara moja shughuli za Bunge Maalum la Katiba ili lisiendelee kufuja mali za Watanzania na kupuuza maoni ya wananchi ...

KIBONDE, GARDNER WAPANDISHWA KIZIMBANI

 Watangazaji Ephraim Kibonde (wa kwanza kushoto) na mwenzake Gardner Habash (wa pili kulia) wakielekea kizimbani. Watangazaji hao wakiongozwa na maofisa wa polisi kuelekea mahakama...

TBL YAKAGUA UJENZI WA KISIMA CHA MAJI CHA ZAHANATI YA MAKUBURI KILICHOJENGWA KWA MSAADA WAO

 Ofisa Uhusiano wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), Dorris Malulu (kushoto), na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mwongozo, James Ngoitanile (wa tatu kushoto) wakiangalia kisima kipya cha ma...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item