MKUTANO WA MAKATIBU WAKUU WA ASASI YA SADC ULIPONGULIWA NA NAIBU KATIBU MKUU

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mkutano wa Makati...

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Mambo ya Nje  wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) akifungua rasmi mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Julai, 2013. Mkutano huo ni maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri utakaofanyika tarehe 13 Julai, 2013.
Wajumbe wa Tanzania wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo. Kulia ni Mhe. Radhia Msuya, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini na Balozi Naimi Aziz, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Balozi Gamaha (wa pili kutoka kushoto) akiwa na Kamishina wa Magereza wa Afrika Kusini, Bw. Tom Moyane (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi Mkuu wa masuala ya Usalama wa Namibia, Bw. Ben Likando (Kulia) na Mkurugenzi wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, Luteni Kanali Mstaafu, Tanki Mothae (kushoto) kabla ya ufunguzi wa mkutano huo.



Wajumbe kutoka nchi wanachama wa SADC wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa Makatibu Wakuu.

Related

TAARIFA KAMILI YA KIFO CHA MTOTO NASRA ALIYEISHI KATIKA BOKSI KISHA KUFARIKI DUNIA HOSPITALI YA MUHIMBILI DAR ES SALAAM YAIBUA SIMANZI NCHINI.

MSIBA wa mtoto Nasra Mvungi (4), aliyeteswa kwa kufungiwa katika boksi kwa zaidi ya miaka minne, ambako ndiko alikokuwa akipewa chakula, kwenda haja kubwa na ndogo na kulala, umeibua simanz...

MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU DAR ES SALAAM (UDSM) AKUTWA AMEFARIKI BAADA YA KWENDA KUPUMZIKA HOSTEL

Mwanafunzi mmoja wa Kike wa Chuo kikuu cha Dar es Salaam leo mchana muda wa saa nane amekutwa amefariki akiwa amelala kitandani chumba cha hostel, Inasemekana aliwaaga wenzake kuwa anakwen...

TASWIRA MBALIMBALI ZA MAZISHI YA MSANII RACHEL HAULE YALIYOFANYIKA JANA KATIKA MAKABURI YA KINONDONI

  Mchumba wa Marehemu Rachel, Saguda (katikati) akiwa na majonzi tele wakati wa mazishi ya mchumba wake  Majeneza yenye mwili wa marehemu Rachel na Mwanae yakiletwa Katika makab...


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904746
item