MKUTANO WA MAKATIBU WAKUU WA ASASI YA SADC ULIPONGULIWA NA NAIBU KATIBU MKUU

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mkutano wa Makati...

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha ambaye pia ni Mwenyekiti wa Mkutano wa Makatibu Wakuu wa Mambo ya Nje  wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC) akifungua rasmi mkutano huo uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Julai, 2013. Mkutano huo ni maandalizi ya Mkutano wa Mawaziri utakaofanyika tarehe 13 Julai, 2013.
Wajumbe wa Tanzania wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo. Kulia ni Mhe. Radhia Msuya, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini na Balozi Naimi Aziz, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Balozi Gamaha (wa pili kutoka kushoto) akiwa na Kamishina wa Magereza wa Afrika Kusini, Bw. Tom Moyane (wa pili kutoka kulia), Mkurugenzi Mkuu wa masuala ya Usalama wa Namibia, Bw. Ben Likando (Kulia) na Mkurugenzi wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya SADC, Luteni Kanali Mstaafu, Tanki Mothae (kushoto) kabla ya ufunguzi wa mkutano huo.



Wajumbe kutoka nchi wanachama wa SADC wakimsikiliza Balozi Gamaha (hayupo pichani) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo wa Makatibu Wakuu.

Related

OTHER NEWS 6036379992598098918

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item