MFANYA BIASHARA ARUSHA AMWAGIWA TINDIKALI

Mfanyabiashara Japhet Minja amelazwa katika Hospitali ya Arusha Lutheran Centre (Seliani) jijini Arusha, baada ya kumwagiwa kimimi...



Mfanyabiashara Japhet Minja amelazwa katika Hospitali ya Arusha Lutheran Centre (Seliani) jijini Arusha, baada ya kumwagiwa kimiminika kinachosadikiwa kuwa tindikali usoni na watu wasiojulikana.

Minja alitendewa unyama huo jana saa 12.15 alfajiri eneo la Shamsi wakati akitoka nyumbani kwake kwenda kazini.
Akisimulia tukio hilo, mmoja wa ndugu wa Minja ambaye hakutaka kutaja jina lake, alidai Minja alikutwa na mkasa huo wakati akiendesha gari lake kwenda katika shughuli zake za kawaida.

Alidai baada ya kufika eneo la Shamsi alikutana na vijana wanne wakiwa wamesimama barabarani, wakamsimamisha kama vile watu waliokuwa wakiomba msaada.
“Baada ya ndugu yangu kusimama, alishusha kioo cha gari upande wake na hapo wale vijana wakafungua mlango kwa nguvu na kumchomoa ndani ya gari na kumtoa nje.
“Baada ya hapo walimshambulia kwa kumpiga na kummwagia tindikali usoni,” alidai.
Alidai baada ya kumwagiwa tindikali, watu waliokuwa karibu na eneo hilo walijaa na vijana hao walikimbia na kutokomea kusikojulikana.
Hata hivyo waandishi waliotembelea Hospitali ya Seliani kuonana na mgonjwa, hawakuruhusiwa kwa madai kuwa mgonjwa huyo yupo chumba cha uangalizi maalum (ICU).

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Liberatus Sabas, akizungumzia tukio hilo alisema kuwa Polisi wanaendelea na uchunguzi.
“Kitu kinachotupa mashaka ni kimoja… yule mtu aliendesha gari mwenyewe, sasa kama ni tindikali utaweza kuendesha gari kweli, hivyo vitakuwa visa tu,” alidai Kamanda Sabas.

Sabas alidai kuwa hata uso wake haujaathirika kama watu wanavyosema, japo ameumia kidole ambacho anadai aling’atwa na watu hao waliomvamia. Alisema kijana huyo anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka 30 ni mfanyabiashara na anatengeneza madirisha ya aluminium.

Related

MWILI WA MAREHEMU WILLIAM MGIMWA WAAGWA VIWANJA VYA KARIMJEE JIJINI DAR ES SALAAM

Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk. William Mgimwa likiwa mbele ya waombolezaji. Rais Jakaya Kikwete pamoja na Mama Salma wakiaga mwili wa marehemu Dk. Mgimwa ...

BOTI YA KILIMANJARO MALI YA AZAM MARINE YAPATA AJALI IKITOKEA PEMBA, MAITI 5 ZAPATIKANA

Boti ya Kampuni ya Azam Marine ya Kilimanjaro  ikitokea Pemba asubuhi ya leo ikiwa na abiria karibu 320 imepata misukosuko ya hali ya upepo na mawimbi na kusababisha baadhi ya abiria wali...

MOTO ULIVYOITEKETEZA JANCO MOTEL ILIYOPO MBEYA JANA USIKU

Jana usiku moto mkubwa ulizuka katika hotel ya Janco iliyopo eneo la Forest Mpya na kuteketeza baadhi ya vitu, chanzo cha moto huo hakijafahamika hadi sasa. Idadi ya vifo na ma...


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904759
item