NEC YATANGAZA UCHAGUZI KWA KATA 27

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kata 27 nchini ambazo zipo wazi kutokana na madiwani wake kufariki dunia na wengine kupoteza s...

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kata 27 nchini ambazo zipo wazi kutokana na madiwani wake kufariki dunia na wengine kupoteza sifa, uchaguzi wake utafanyika Februari 9 mwakani.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mkurugenzi wa NEC, Julius Mallaba, alisema uchaguzi huo utafanyika katika halmashauri 23 baada ya kukamilisha taratibu zinazotakiwa.

Alizitaja kata hizo na halmashauri zake zikiwa kwenye mabano ni Segela na Mpwayungu (Chamwino), Ukumbi na Ibumu (Kilolo), Nduli (Iringa), Malindo (Rungwe) na Santilya (Mbeya).

Nyingine ni Tungi (Morogoro), Mkwiti (Tandahimba), Mkongolo (Kigoma), Sombetini (Arusha), Mrijo (Chemba), Magomeni na Kibindu (Bagamoyo), Mtae (Lushoto), Ubagwe (Ushetu) na Namikago (Nachingwea).

Kata nyingine ni Partimbo na Loolera (Kiteto), Kiwalala (Lindi), Kilelema (Buhigwe), Kiomoni (Tanga), Kasanga (Kalambo), Rudewa (Kilosa), Kiborloni (Moshi), Njombe Mjini (Njombe) na Nyasura (Bunda).

Alisema uteuzi wa wagombea udiwani utafanyika Januari 15, wakati kampeni za uchaguzi zitaanza Januari 16 hadi Februari 8 na siku ya kupiga kura itakuwa Februari 9.

Alipoulizwa kama Kata ya Kisesa iliyopo Mwanza itaingizwa katika uchaguzi huo baada ya aliyekuwa diwani wake, Clement Mabina kuuawa na wananchi, alisema haitaingizwa katika uchaguzi huo.

Alisema utafanyika baada ya Halmashauri ya Ilemela kupeleka maombi ya kuomba uchaguzi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Related

MGOMO WA MASHINE ZA EFD WASITISHWA

Wafanyabiashara katika mikoa mbalimbali leo wamefungua maduka yao ikiwemo kariakoo, Tanga na Kahama. Hii imekuja baada ya kufanyika kikao baina ya wafanyabiashara na Waziri Mkuu jana. Matokeo ya ki...

OKWI RUKSA KUICHEZEA YANGA

Shirikisho la soka la kimataifa (FIFA) limemuidhinishia Emmanuel Okwi kuichezea timu ya Yanga, TFF imethibitisha swala hilo. Source: Mwananchi

SEHEMU YA MAJENO YA CHUO CHA POLISI MOSHI CCP YAUNGUA MOTO, TAZAMA PICHA

 Wanafunzi wa chuo cha taaluma ya polisi Moshi wakijaribu kuzima moto na kuokoa mali zilizokuwa zikiungua katika moja ya stoo ya kuhifadhia vitu mbalimbali zikiwemo nguo baada ya kuzuka kw...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904759
item