NEC YATANGAZA UCHAGUZI KWA KATA 27

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kata 27 nchini ambazo zipo wazi kutokana na madiwani wake kufariki dunia na wengine kupoteza s...

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kata 27 nchini ambazo zipo wazi kutokana na madiwani wake kufariki dunia na wengine kupoteza sifa, uchaguzi wake utafanyika Februari 9 mwakani.

Akizungumza na Tanzania Daima jana, Mkurugenzi wa NEC, Julius Mallaba, alisema uchaguzi huo utafanyika katika halmashauri 23 baada ya kukamilisha taratibu zinazotakiwa.

Alizitaja kata hizo na halmashauri zake zikiwa kwenye mabano ni Segela na Mpwayungu (Chamwino), Ukumbi na Ibumu (Kilolo), Nduli (Iringa), Malindo (Rungwe) na Santilya (Mbeya).

Nyingine ni Tungi (Morogoro), Mkwiti (Tandahimba), Mkongolo (Kigoma), Sombetini (Arusha), Mrijo (Chemba), Magomeni na Kibindu (Bagamoyo), Mtae (Lushoto), Ubagwe (Ushetu) na Namikago (Nachingwea).

Kata nyingine ni Partimbo na Loolera (Kiteto), Kiwalala (Lindi), Kilelema (Buhigwe), Kiomoni (Tanga), Kasanga (Kalambo), Rudewa (Kilosa), Kiborloni (Moshi), Njombe Mjini (Njombe) na Nyasura (Bunda).

Alisema uteuzi wa wagombea udiwani utafanyika Januari 15, wakati kampeni za uchaguzi zitaanza Januari 16 hadi Februari 8 na siku ya kupiga kura itakuwa Februari 9.

Alipoulizwa kama Kata ya Kisesa iliyopo Mwanza itaingizwa katika uchaguzi huo baada ya aliyekuwa diwani wake, Clement Mabina kuuawa na wananchi, alisema haitaingizwa katika uchaguzi huo.

Alisema utafanyika baada ya Halmashauri ya Ilemela kupeleka maombi ya kuomba uchaguzi kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)

Related

DKT. KITILA NA MWIGAMBA WAVULIWA UANACHAMA NDANI YA CHAMA CHA CHADEMA

DKT. KITILA MKUMBO SAMSON MWIGAMBA KAMATI Kuu ya Chadema iliyokutana Januari 3 - 4, 2014 katika Ukumbi wa Mbezi Garden, jijini Dar es Salaam imeamua kuwavua uanachama Dkt. Kitila Mkumbo...

MWILI WA MAREHEMU WILLIAM MGIMWA WAAGWA VIWANJA VYA KARIMJEE JIJINI DAR ES SALAAM

Jeneza lenye mwili wa aliyekuwa Waziri wa Fedha na Uchumi, Dk. William Mgimwa likiwa mbele ya waombolezaji. Rais Jakaya Kikwete pamoja na Mama Salma wakiaga mwili wa marehemu Dk. Mgimwa ...

BOTI YA KILIMANJARO MALI YA AZAM MARINE YAPATA AJALI IKITOKEA PEMBA, MAITI 5 ZAPATIKANA

Boti ya Kampuni ya Azam Marine ya Kilimanjaro  ikitokea Pemba asubuhi ya leo ikiwa na abiria karibu 320 imepata misukosuko ya hali ya upepo na mawimbi na kusababisha baadhi ya abiria wali...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904765
item