MWALIKO KWA MAKUNDI MBALIMBALI KUPENDEKEZA MAJINA YA WATAKAOTEULIWA KUWA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA

UNITED REPUBLIC OF TANZANIA TANZANIA INFORMATION SERVICES PRESS RELEASE                P.O. Box 9142, Dar es Salaam, Te...

TANZANIA INFORMATION SERVICES

PRESS RELEASE
               P.O. Box 9142, Dar es Salaam, Tel:  2110585, 2122771/3, Fax: 2113814,
 e-mail: 
 Date:  20/12/2013

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
 
 MWALIKO KWA MAKUNDI MBALIMBALI KUPENDEKEZA MAJINA YA WATAKAOTEULIWA KUWA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete  anapenda kutoa mwaliko kwa makundi mbalimbali kwa ajili ya kuwasilisha orodha ya watu wasiopungua wanne na waziozidi tisa kwa ajili ya kuteuliwa kuwa wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba kwa mujibu wa kifungu kidogo cha (2A) cha kifungu cha 22 cha sheria ya Mabadiliko ya Katiba, sura ya 83 kinachomtaka Rais kuwaalika kila kundi lililoainishwa chini ya kifungu kidogo cha (1) (c) kutoka pande zote za Muungano kuwasilisha kwake orodha ya majina yasiyopungua 4 na yasiozidi 9 kwa ajili ya kuzingatiwa katika uteuzi.

Makundi hayo ni kama ifuatavyo:

Taasisi zisizokuwa za Kiserikali
Taasisi za kidini
Vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu
Taasisi  za elimu ya juu
Makundi yenye ulemavu
Vyama vya wafanyakazi
Vyama vinavyowakilisha wafugaji
Vyama vya wakulima
Vyama vinavyowakilisha wavuvi
Makundi mengine yenye malengo yanayofanana

Katika kuwasilisha majina hayo, makundi yaliyoalikwa yatalazimika kuonesha umri, jinsia, uzoefu, sifa na sehemu ya makazi ya mtu aliyependekezwa ikiwa ni pamoja na kuzingatia usawa wa kijinsia.

Mheshimiwa Rais ameelekeza kuwa orodha ya majina yanayopendekezwa yawasilishwe kwa maandishi ama kwa kupeleka kwa mkono au kutumia huduma ya posta kwa anuani zifuatazo:

Katibu Mkuu Kiongozi,
Ofisi ya Rais, Ikulu,
S.L.P. 9120,
DAR ES SALAAM

Katibu Mkuu Kiongozi,
Ofisi ya Rais,
S.L.P. 4224,
ZANZIBAR

Mwisho wa kupokea orodha ya majina hayo nitarehe 02 Januari, 2014.

Related

MBUNGE WA CCM JIMBO LA BAHI AKUMBWA NA KASHFA NZITO KATIKA MFUKO WA JIMBO MKOANI DODOMA

DODOMA.  MBUNGE wa Bahi (CCM), Omar Badwel ameingia katika kashfa baada ya Kamati ya Uhakiki wa Fedha za Mfuko wa Maendeleo ya Jimbo kubaini matumizi mabaya ya fedha hizo. Kamati hiyo il...

KATIBU MKUU WA UN AONYA KUHUSU GHASIA AFRIKA YA KATI (CAR)

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon ameonya kuwa ghasia zinazoendelea katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, zinaweza kuligawa taifa hilo na kuwatenga kabisa Wakristo na Waislamu. Bwana B...

CCM YATEUA MGOMBEA WAKE UCHAGUZI MDOGO JIMBO LA KALENGA

     Dar es salaam. Kamati Kuu ya CCM, chini ya Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete, imempitisha Godfrey William Mgimwa kugombea ubunge kwa tiketi ya CCM, katika uchaguzi mdo...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904776
item