MWALIKO KWA MAKUNDI MBALIMBALI KUPENDEKEZA MAJINA YA WATAKAOTEULIWA KUWA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA
UNITED REPUBLIC OF TANZANIA TANZANIA INFORMATION SERVICES PRESS RELEASE P.O. Box 9142, Dar es Salaam, Te...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Makundi hayo ni kama ifuatavyo:
Taasisi zisizokuwa za Kiserikali
Taasisi za kidini
Vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu
Taasisi za elimu ya juu
Makundi yenye ulemavu
Vyama vya wafanyakazi
Vyama vinavyowakilisha wafugaji
Vyama vya wakulima
Vyama vinavyowakilisha wavuvi
Makundi mengine yenye malengo yanayofanana
Katika kuwasilisha majina hayo, makundi yaliyoalikwa yatalazimika kuonesha umri, jinsia, uzoefu, sifa na sehemu ya makazi ya mtu aliyependekezwa ikiwa ni pamoja na kuzingatia usawa wa kijinsia.
Mheshimiwa Rais ameelekeza kuwa orodha ya majina yanayopendekezwa yawasilishwe kwa maandishi ama kwa kupeleka kwa mkono au kutumia huduma ya posta kwa anuani zifuatazo:
Katibu Mkuu Kiongozi,
Ofisi ya Rais, Ikulu,
S.L.P. 9120,
DAR ES SALAAM
Katibu Mkuu Kiongozi,
Ofisi ya Rais,
S.L.P. 4224,
ZANZIBAR
Mwisho wa kupokea orodha ya majina hayo nitarehe 02 Januari, 2014.