MSAADA UNAHITAJIKA KWA MTOTO GRACE

Grace ni mtoto wa miaka 14,mwenye uzito wa kilo 111.kwa zaidi ya miaka kumi Grace amekua akiishi maisha ya tabu,shida na maumivu makali...

Grace ni mtoto wa miaka 14,mwenye uzito wa kilo 111.kwa zaidi ya miaka kumi Grace amekua akiishi maisha ya tabu,shida na maumivu makali kimwili na kisaikologia yaliyoletwa na uzito mkubwa /unene alionao.Alilazimika kuacha shule akiwa darasa la nne baada yakushindwa kukabiliana na unyanyapaa aliokutana nao katika maisha yake yakila siku,hasa shuleni na barabarani.
Grace alizaliwa na afya nzuri na alifurahia maisha yake kama watoto wengine ,Ingawa alianza kunenepa akiwa na miaka miwili unene wake ulikua wakaaida. Hali ilibadilika alipofikisha miaka mitano ambapo alinenepa sana,na unene wake haukua wakawaida kwani ulikua unene wakuvimba mwili.Siku hadi siku Grace alizidi kuongezeka adi kufikia hivi alivyo leo.
Hali hii ya unene iliambatana na matatizo mengine ya afya ,aliumwa sana kichwa hasa sehemu ya paji la uso na wakati mwingine alihisi kichwa kizito sana.Alipata shida kupumua na wakati mwingine alilazimika kulala milango na madirisha yakiwa wazi.Miguu yake ilikua na maumivu wakati wote
Grace Alipelekwa hospitali kwa ajili ya matibabu,na alipewa rufaa mwenda hospitali ya mwimbili kwa ajili ya uchunguzi wa kina na matibabu mwaka 2010.Kwa bahati Mbaya Gharama za vipimo zilikua kubwa sana na wazazi wake hawakua na uwezo wakulipa gharama hizo za shilingi laki nane.
Wazazi walijitahidi na kumpeleka katika hospitali zingine ambazo waliweza kumudu garama zake,huko alifanyiwa uchunguzi mdogo,uchunguzi huo ulibaini kua ,moyo wake umezungukwa na mafuta mengi,maini yake yanasumu nyingi,mishipa yake ya damu inamafuta mengi na homoni zake pia zinatatizo.Alipata matibabu ya dawa zenye asili ya chakula,ambazo anatumia adi sasa.
Nilipoongea na Mtoto Grace aliniambia anatamani sana kurudi shule ilia some nakutimiza ndoto yake yakua Daktari.Nilipomuuliza juu ya unyanyapaa anaokabiliana kila siku,alisema “wananiita majina mabaya,bonge nyanya,fupi nyundo,chabunene,alafu wengine wananifunua nguo wananichungulia na kunicheka,sikunyingine wananimwagia michanga” Haya si maisha yanayomsahili mtoto huyu.
Afya ya Grace si njema,bado anakabiliwa na changamoto zote zilizoelezwa hapo juu. Anahitaji msaada wa matibabu ili kunusuru afya na maisha yake.
Tollyzkitchen kupitia kampeini yake ya PUNGUZA KILO MOJA ambayo ni maalumu kwa ajili yakupunguza uzito na kukabiliana na magonjwa yasababishwayo na unene na chakula ,tunafanya juhudi za kuchangisha fedha ili kumsaidia mtoto huyu
Ukiwa kama mpenzi na mtumiaji wa jiko hili,naomba uungane nasi katika kumsaidia mtoto huyu.Msaada wako wowote niwathamani sana kwake na kwetu pia , uwezo wakumpa maisha anayoyatamani uko mikononi mwako .
Tumia namba hii kutuma msaada wako O713 755 741,ukituma Tigo pesa itaandika majina:AKII CHAWACHI. Mpesa 0769 003 955 itaandika majina SAUDA MBARUK 
Tunatanguliza shukurani na Mungu akubariki,akuzidishie pale ulipotoa.
Tutatoa maendeleo ya Mtoto Grace kupitia www.tollyzkitchen.wordpress.com au www.tollyben.com kadri tutakavyokua tunafanikiwa katika kumsaidia.

Related

DKT. ASHA - ROSE MIGIRO AAPISHWA BUNGENI LEO

MBUNGE wa kuteuliwa na Rais,  Dk. Asha-Rose Migiro, leo saa 3 asubuhi, ameapishwa kuwa mbunge wa Bunge la Tanzania. Akizungumza nje ya viwanja vya Bunge, baada ya kuaspishwa, na Spika wa Bun...

The most exclusive flight in the world: Behind-the-scenes photos from Air Force One show the Obamas mingling with the Bushes and Hillary on journey to South Africa for Mandela's memorial

Impressed: Former President Bush shows photos of his paintings to, from left, Michelle Obama, Hillary Clinton, Advisors Valerie Jarrett and Susan E. Rice, Attorney General Eric Holder and Laura ...

BAADA YA KUVULIWA CHEO: ZITTO AKATA RUFAA BARAZA KUU LA CHADEMA

TAARIFA iliyotolewa jana December 11 2013 na Albert Msando ambae ni Mwanasheria wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini Zitto Kabwe kuhusu zile headlines za hivi karibuni za kuvuliwa vyeo CHADEMA imesema ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904970
item