BUNGE LA KATIBA KUAHIRISHWA APRILI 28

  MWENYEKITI wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, jana alikutana na viongozi wa dini za Kiislamu na Kikirstu, kuzungumzia msugua...


 MWENYEKITI wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta, jana alikutana na viongozi wa dini za Kiislamu na Kikirstu, kuzungumzia msuguano wa bunge la katiba unavyoendelea bungeni.
Asubuhi alikutana na kiongozi wa Kanisa Katoliki, Muadhama Kadinali Pengo katika kanisa la la Mt.Joseph jijini Dar es Salaam na baadae akakutana na Mufti Mkuu wa Tanzania, Sheikh Issa bin Shaaban Simba katika ofisi za Bakwata.
Mazungumzo yao yalijikita zaidi katika mchakato wa bunge la katiba unaosuasua kutokana na misimamo ya kisiasa na kuwaomba viongozi hao kuuombea mchakato huo ukwamuke.
Akizungumza na Sheikh Shaaban bin Simba, Sitta, alisema katiba mpya ni kwa manufaa ya wanachi wote kwa ajili ya kuwaletea maendeleo katika nyanja mbalimbali.
Alisema viongozi wa dini ni watu muhimu kwakuwa wanabeba wafuasi wengi katika jamii na kuwepo kwao kunasaidia katika maendeleo ya nchi hususani kujenge amani na kuwahamasisha wananchi kuwa wavumilivu, watulivu,waelewa na wenye kupenda amani.
“Namuomba Mhe.Mufti Shaaban bin Simba pamoja viongozi wengine wa dini wazidi kutuombea ili tuweze kufikia muafaka katika kupata katiba mpya na bora yenye kuleta mabadiliko katika nchi yetu,” alisema.

Aidha alisema Watanzania wanataka katiba itakayojenga taasisi imara zitakazosimamia mambo muhimu na kuondokana na uhalifu ikiwemo janga la dawa za kulevya ambalo limekuwa likiisumbua nchi.
Aliwaomba wajumbe wa kamati 12 za bunge la katiba, wasome kwa makiini ibara ya sura ya 1 na ya 6 ambazo ni muhimu katika kujenga nchi, ili waweze kutoka na mawazo mazuri na yakinifu  kwa manufaa ya nchi na watu wake.
“Katiba itunge sheria ambazo ni imara zenye kufuata kanuni na taratibu dhabiti ili kuleta mabadiliko katika kuiongoza nchi na kuweza kuwasaidia wananchi wake,” alisema.
Aidha, alisema bunge hilo linatarajia kuahirishwa Aprili 28 kwa ajili ya kupisha bunge la bajeti na kwa kuwa siku  70 hazitoshi kumaliza bunge hilo amemuomba Rais kuwaongezea muda hivyo wanatarajia kurudi tena mwezi wa Ogasti kuendelea na mijadala ya katiba mpya.

Akizungumza na Kadinali Pengo, Sitta alimuomba kuliombea bunge ili kufikia muafaka na kutoka na katiba mpya na bora yenye kuleta mabadiliko.

Related

DKT. SHEIN ZIARANI NCHINI INDIA

STATE HOUSE ZANZIBAR OFFICE OF THE PRESS SECRETARY PRESS RELEASE     Zanzibar                &nb...

ASKARI POLISI 5 WAFARIKI DUNIA DODOMA, SOMA MAJINA YAO HAPA

Ajali mbaya ya kusikitisha imetokea Jana usiku majira ya saa nane ambapo gari ya ya polisi iliyokuwa inatoka Dodoma kwenye sherehe ya polisi iliyokuwa inafanyika katika ukumbi wa mipango. ...

JAJI MKUU AISHUKIA TUME YA MAREKEBISHO YA SHERIA TANZANIA

  DAR ES SALAAM. JAJI Mkuu Mohamed Othman Chande ameitaka Tume ya Kurekebisha Sheria Tanzania kuharakisha mchakato wake wa kuandaa ripoti inayohusu migogoro ya ardhi nchini ili kutoa nafas...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item