MTWARA HALI SI SHWARI

Ni magari ya FFU tu ndio yapo barabarani nayo hupata wakati mgumu kupita kwasababu ya mawe na magogo yaliyowekwa na vijana,baadhi ya watu ...



  • Ni magari ya FFU tu ndio yapo barabarani nayo hupata wakati mgumu kupita kwasababu ya mawe na magogo yaliyowekwa na vijana,baadhi ya watu kadhaa wamechukuliwa na askari eti kwakuwa walipita jirani na gari yao,askari wengi waliokuja si wa hapa Mtwara wengi wametoka Masasi na Lindi. Ving'ora vinalia ovyo ovyo.


  • watoto wamefungiwa mashuleni walimu wamekimbia

  • Vituo vya Redio vya Mtwara havizungumzii hali hii ya hatari. Vinapiga Muziki pengine vinakusanya matukio na habari ya majanga haya. Ili Wananchi wayapate .

  •  Mabomu yanapigwa mfululizo maeneo ya Magomeni-Mtwara . Takriban mabomu 20 na ushee mpaka sasa. Na wanaendelea kupiga mabomu.
  • Sasa hali si shwari kila eneo, wakionekana watu watatu wanaongea maongezi maaskari wanapiga mabomu. Mabavu yamechukua mkondo wake. Wananchi wamejifungia majumbani mwao. Chuki dhidi ya Polisi yaimarika. Polisi wanapiga mabomu bila mwelekeo.
  • Magomeni na sokoni kimenuka, mabomu yanarushwa na wananchi wanakimbia ovyo.

  • Kituo  kimoja  cha habari  kinachorusha habari za bunge chazuia mawimbi yake kwa Mkoa wa Mtwara hivyo hakisikiki(Redio na TV). Na kimewanyima haki wananchi wa Mtwara ya kupata taarifa.(Hatimaye wamerejesha matangazo yao)

  • Waziri wa Nishati amesoma hotuba yake kwa hisia kali na mbwembwe. Mwishoni amesema bomba la gesi linajengwa kutoka Mtwara kwenda Dar.


  • Maduka yote yamefungwa, baa zimefungwa, hakuna huduma za usafiri, ofisi za serikali zimepwaya kimsingi hakuna lolote linalofanyika
  • Boda boda zinazoonekana maeneo ya Nkanaledi na abiria zinapigwa mawe.


  • Makachero nao wanajifanya madereva wa boda boda na Bajaji, Tax wengine wanatembea na magari ya Serikali.


  • Maeneo yote yametawaliwa na ukimya.


  • Kesho inaendelea tena kwa siku ya pili.  
  • Serikali  isipoangalia inaweza ikasababisha "Uprising" maeneo mengine ya nchi.


SOURCE: Mtwarakumekucha

Related

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL AFUNGUA KONGAMANO LA UHAMASISHAJI NA UWEKEZAJI KANDA YA ZIWA JIJINI MWANZA.

   Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akihutubia wakati wa ufunguzi rasmi wa Kongamano la siku tatu la Uwekezaji na Uhamasishaji Kanda ya Z...

KAMATI KUU CHADEMA KUKUTANA KWA DHARURA

    TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KAMATI KUU YA CHADEMA KUKUTANA KWA DHARURA   Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana kwa ajili ya kikao ch...

KAMATI KUU CCM YAWAHOJI WATATU JANA

 Waziri Mkuu wa Zamani Ndugu Fredrick Sumaye akiwasili kwenye Makao Makuu ya Chama Cha Mapinduzi Dodoma tayari kwa kuhojiwa na Kamati Ndogo ya Maadili.  Waziri Mkuu Mstaafu Ndugu E...

Newer Post UNYWELE
Older Post DECOR

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904812
item