BUNGE MAALUM LAANZA KUSIKILIZA TAARIFA ZA KAMATI

Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta amesema mjadala kuhusu  taarifa za Sura ya Kwanza na ya Sita za Rasimu  ya  Katib...



Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba, Samuel Sitta amesema mjadala kuhusu  taarifa za Sura ya Kwanza na ya Sita za Rasimu  ya  Katiba  ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania unatarajia kuanza wiki ijayo katika Bunge hilo mara baada ya kumaliza kupokea taarifa za Kamati.

 Sitta  alisema hayo  katika ukumbi wa Bunge hilo mjini Dodoma baada  baadhi ya wajumbe kumwomba  kuchangia mjadala wakati ripoti hizo zikiendelea kuwasilishwa.

 Alisema mdajala wa kuchangia sura hizo utaanza mara baada  ya   Kamati 12 za Bunge Maalum la Katiba  kuwasilisha  taarifa zao  za Sura ya Kwanza na ya Sita  kuhusu  Rasimu ya  Katiba  ya Jamhuri ya Muungano  wa Tanzania katika Bunge hilo.

 Aliongeza kuwa  kwa kujibu wa Kanuni ya namba 33(6) ambayo inasema baada ya  hoja za taarifa za Kamati  Namba Moja  hadi Namba Kumi na Mbili kutolewa katika Bunge Maalum na Mwenyekiti kuelekeza hoja hizo zijadiliwe , mjadala kuhusu taarifa hizo utaanza.

 Mwenyekiti huyo aliwataka baadhi ya wajumbe hao kusubiri mpaka uwasilishaji wa taarifa hizo utakapokamilika ndio watapata nafasi  ya kuchangia kwa muda mrefu  na kuwezesha wajumbe wengi kupata nafasi hiyo.
 (Picha na Bunge Maalum la Katiba)

Related

OTHER NEWS 8288312199216904418

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item