KUELEKEA UCHAGUZI MDOGO CHALINZE: VYAMA VYASHAURIWA KUWATUMIWA MAWAKALA WA JIMBO HUSIKA

  Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,Jaji Mstaafu Damiani Lubuva TUME ya Taifa ya uchaguzi imevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki kwe...

 Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi,Jaji Mstaafu Damiani Lubuva

TUME ya Taifa ya uchaguzi imevitaka vyama vya siasa vinavyoshiriki kwenye Uchaguzi Mdogo wa Jimbo la Chalinze kuhakikisha kuwa wanawatumia mawakala wanaotoka katika maeneo au vituo husika vya kupigia kura,ambao watawafahamua na kuwatambua wapiga kura wa eneo husika. 

Akizungumza katika mkutano baina ya vyama vya siasa na tume hiyo,Mwenyekiti wa Tume hiyo,Jaji mstaafu Damiani Lubuva amesema kuwa pamoja na kuwa sheria haikatazi kwa vyama kuteua mawakala wa vyama kutoka majimbo mengine ya uchaguzi,lakini ni vyema kuwateua wale wanaotoka katika maeneo hayo ili kuweza kuwatambua wapiga kura wao. 

“Kumekuwa na mazoea kwa baadhi ya vyama vya siasa kuteua mawakala wanaotoka majimbo mengine ya uchaguzi japokuwa sheria haikatazi lakini ni vema vyama vikatumia busara  ya kuwateua mawakala kutoka katika maeneo hayo ili kuweza kuwatambua wapiga kura” alisema Jaji Lubuva. 

Akizungumzia kuhusu umuhimu wa wananchi kujitokeza kupiga kura,Lubuva alisema kuwa tume inatambua juhudi za viongozi wa vyama vya siasa kuwahamasisha wananchi kujitokeza kushiriki katika uchaguzi lakini akawataka viongozi hao kuhakikisha kuwa wanawahamasisha zaidi wapiga kura kujitokeza kwa wingi siku ya kupiga kura. 

Akizungumzia kuhusiana na maandalizi ya uchaguzi huo mdogo wa Chalinze,Msimamizi msaidizi wa uchaguzi wa jimbo hilo,ambaye pia ni Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo Samweli Sarianga alisema kuwa vifaa vyote na maandalizi yamekamilika japokuwa kumekuwako na changamoto nyingi ikiwamo uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha hivi karibuni na kusisitiza kuwa iwapo hali ya hewa itakuwa ni nzuri basi kuna uhakika wa vifaa vyote vya uchaguzi vitakuwa vimefikishwa katika maeneo husika tayari kwa ajili ya kusambazwa katika vituo vya kupigia kura. 

Jumla ya vyama 5 vinatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huo mdogo wa Chalinze ambapo lina idadi ya wapiga 92,939,ambapo vyama hivyo ni CCM,CHADEMA,NRA,CUF na AFP.

Related

AJALI YA PIKIPIKI NA MAGARI YAUA WATU WATATU

 Mifuko maalumu ya kuzuia abiria asiumie wakati wa ajali ikiwa imefumuka baada ya ajali .    Gari aina ya Range Rover lenye likiwa limeharibika vibaya ba...

NAIBU WAZIRI WA MAJI ATEMBELEA MIRADI YA MAJI MIKOA YA PWANI NA DAR ES SALAAM

 Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla akiambatana na wakandarasi wa kampuni ya WABAG pamoja na Meneja Mradi DAWASA, Inj. Romanus Mwang’ingo (mwisho kulia) wakikagua mradi wa maji wa Ruvu ...

MBUNGE GODFREY MGIMWA AKABIDHI MSAADA WA BATI KIJIJI CHA USENGERENDETI NA MAHANZI

 Katibu  wa mbunge  wa jimbo la Kalenga  Bw  Martine Simangwa  kushoto akikabidhi msaada wa bati  100 kwa  uongozi wa kijiji cha Usengerendeti  kwa &...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item