Majaji EACJ waruhusu Spika Eala kung’olewa

Spika wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala), Dk Magreth Zziwa Arusha.  Spika wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala), Dk Magreth Zziwa a...

Spika wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala), Dk Magreth Zziwa

Arusha. 
Spika wa Bunge la Afrika Mashariki (Eala), Dk Magreth Zziwa amekalia kuti kavu kutokana na uwezekano wa kung’olewa madarakani baada ya Mahakama ya Afrika Mashariki (EACJ), kuruhusu bunge hilo kuendelea na shughuli zake kulingana na kanuni na taratibu zake.
Jopo la majaji watatu wa EACJ, wakiongozwa na Jaji Mfawidhi Jean-Bosco Butasi lilitupilia mbali maombi ya zuio la muda kuhusu Kanuni za Bunge zinazohusu suala la kumwondoa madarakani spika lililowasilishwa na Taasisi ya Mbidde Foundation Ltd ya nchini Uganda na Spika Zziwa mwenyewe.
Wabunge wa Eala wanataka kumng’oa Spika Zziwa kwa madai ya kupendelea makundi na dharau miongoni mwa wabunge, matumizi mabaya ya madaraka na kushindwa kumudu majukumu yake.
Mwanzoni mwa Aprili, bunge la Eala lilivunjika baada ya kuibuka malumbano kati ya makundi mawili yanayosigana, moja likitaka kumng’oa Spika na jingine likimtetea.
Zziwa ni Spika wa tatu wa bunge la Eala na wa kwanza mwanamke kukalia kiti hicho. Spika wa kwanza alikuwa Abdulrahama Kinana wa Tanzania aliyefuatiwa na Abdirahin Haithar Abdi kutoka Kenya.
Katika uamuzi wao wenye kurasa 16, Jaji Butasi na wenzake, Jaji Isaac Lenaola na Jaji Monica Mugenyi walisema baada ya kupitia hoja za pande zote mbili za wadai na wadaiwa, mahakama imejiridhisha kuwa wadai wa kwanza na wa pili, hawatapata madhara makubwa iwapo zuio la muda lisipotolewa.
Madai ya msingi yaliyopo mbele ya mahakama katika maombi yao ya msingi, taasisi ya Mbidde Foundation Ltd na Spika Zziwa wanaiomba mahakama kutoa ufafanuzi kuhusu uhalali wa kanuni na taratibu za uendeshaji wa Bunge la Eala wakijielekeza katika kanuni ya tisa inayoelekeza jinsi ya kumwondoa madarakani Spika wakidai zinakiuka baadhi ya vifungu vya katiba ya kuanzishwa EAC.
Mdaiwa wa kwanza katika shauri hilo ni Katibu Mkuu wa EAC, Dk Richard Sezibera anayewakilishwa na Mawakili Wilbert Kaahwa na Stephen Agaba, wakati Mwanasheria Mkuu wa Uganda, ambaye ni mdaiwa wa pili akiwakilishwa na jopo la mawakili watatu, Christine Kaahwa, Oburu Odoi na Madete Geofrey.

Wabunge wa Eala wameanza utaratibu wa kumwondoa madarakani Spika kwa kuwasilisha hoja iliyosainiwa na wabunge zaidi ya wanne kutoka kila nchi mwanachama.

Related

NAFASI ZA UBUNGE CHADEMA KUTANGAZWA MAGAZETINI 2015

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimetangaza mfumo mpya wa kuwapata wagombea nafasi ya ubunge kuanzia uchaguzi wa 2015. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU TUKIO LA MLIPUKO KANISANI ARUSHA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI  MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) ametuma salaam za pole na rambirambi kwa waumini wa Kanisa Katoliki nchini na Watanzania wote kwa ujumla k...

HOTUBA YA MSEMAJI MKUU WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI MHE. VINCENT JOSEPHAT NYERERE (MB) KUHUSU MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA 2012/2013 NA MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KATIKA WIZARA YA MAMBO YA NDANI YA NCHI KWA MWAKA WA FEDHA 2013/2014

UTANGULIZI Mheshimiwa Spika,kwa Mujibu wa Kanuni ya 99(9) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, toleo la 2013; napenda kuchukua fursa hii kuwasilisha maoni ya Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni inayoongozwa...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904759
item