RAIS GOODLUCK JONATHAN WA NIGERIA AAHIDI WASICHANA WALIOTEKWA NYARA KUWA WATAPATIKANA

Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, amezungumza wazi kwa mara ya kwanza kuhusu kutekwa kwa waschana takriban 200 wa shule kaskazini ...


Rais wa Nigeria, Goodluck Jonathan, amezungumza wazi kwa mara ya kwanza kuhusu kutekwa kwa waschana takriban 200 wa shule kaskazini mashariki mwa nchi hiyo.

Katika taarifa yake ya kwanza hadharani tangu wasichana 200 kutekwa nyara na watu wanaoshukiwa kuwa wapiganaji wa Waislamu wenye itikadi kali wa Boko Haram, Rais Goodluck Jonathan, amesema kuwa kila juhudi zinapaswa kufanywa kuwakomboa wasichana hao.
Tangazo la Rais lilitolewa kufuatia shinikizo zilizotolewa na familia, makundi ya wanawake na watu wengine ambao wameitaka Serikali kufanya bidii zaidi kuhakikisha kuwa wasichana hao wanakombolewa.

Rais alisema kuwa maafisa wa usalama wamekuwa wakitafuta kila mahali wakitumia ndege na helikopta lakini akakiri kuwa hawajafaulu kutambua walikofichwa wasichana hao.

Alisema kuwa Serikali yake imelazimika kuomba msaada katika kuwatafuta wasichana hao kutoka Serikali za Marekani, Uingereza na Uchina.

Jeshi la Nigeria limekuwa likipambana na kundi hilo la wapiganaji tangu mwaka 2009, lakini mashambulizi na milipuko ya mabomu yameendelea kusikika kila mahali bila kukoma.

Hivi majuzi kumekuwa na milipuko katika mji mkuu wa Abuja katika muda wa majuma matatu ambapo karibu watu 90 waliuawa na wengine wengi kujeruhiwa.

Mnamo Jumatano Kongamo la Dunia juu ya Uchumi wa Afrika utafanyika mjini Abuja na swala la usalama limewatia maafisa wa usalama tumbo joto, ambapo imetangazwa kuwa siku hiyo shule zote na afisi za Serikali zitafungwa ili kuimarisha usalama eneo hilo la mkutano.

Related

IKULU YAKANUSHA HABARI ZA GAZETI LA MWANANCHI YA RAIS KIKWETE KUMTEMBELEA MFUNGWA WA EPA BWANA MARANDA MUHIMBILI

 Rais Jakaya Mrisho Kikwete alipotembelea Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Upasuaji wa Mishipa ya Fahamu (MOI) katika  Hospitali ya Taifa ya Muhimbili jana (Jumamosi) kuwajulia hali wanahab...

UENYEKITI BUNGE LA KATIBA: CCM YAMPITISHA SAMWEL SITTA

  KAMATI ya Uongozi ya Chama Cha Mapinduzi ( C C.M ) imempitisha Waziri wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta, kwa kauli moja kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa Bunge Maalumu la Katiba.Pia kamat...

MFUASI WA ZITTO AANZISHA CHAMA

 Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mwigamba alisema mchakato wa kuandikisha wanachama mikoani kwa ajili ya kuomba usajili wa kudumu kwa mujibu wa sheria umeshakamilika.PICHA|MAKTABA...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904746
item