UPOTOSHWAJI WA TAARIFA YA HALI MBAYA YA HEWA

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA WIZARA YA UCHUKUZI        MAMLAKA YA HALI YA HEWA Simu: +255 22 2460706-8 Telefax: +2...

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
WIZARA YA UCHUKUZI
       MAMLAKA YA HALI YA HEWA



Simu: +255 22 2460706-8
Telefax: +255 22 2460735, 2460700                                                                                                 S.L.P.   3056,
Barua pepe: met@meteo.go.tz                                                                                                          DAR  ES SALAAM
Tovuti: www.meteo.go.tz
                                                                                                                           05/05/2014
                             TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH : UPOTOSHWAJI WA TAHADHARI YA HALI YA HEWA KUHUSIANA NA MVUA ZINAZOENDELEA KUNYESHA
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini inapenda kukanusha kuhusiana na taarifa ya ujumbe mfupi wa simu na katika mitandao ya kijamii wenye maneno yafuatayo : ‘TMA warning heavy rains of strong easterly winds 100km an hour expected to hit Dar coast from Somalia, Heavy rains 120mm above sea level expected today and tommorrow. People must avoid Sea and areas near to Sea should be alert cautioned. Tanzania Meteorological Agency  www.tma.gov.tz’   
Mamlaka inapenda kuutaarifu umma kuwa taarifa hiyo siyo ya kweli  na ina  lengo la kupotosha umma na wala haijatolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania.
Mamlaka ina kuwakumbusha wananchi wote kuendelea kufuatilia taarifa zetu kupitia vyanzo husika vya Mamlaka vikiwemo utabiri wa kila siku utolewao kupitia radio, televisheni na tovuti ya Mamlaka (www.meteo.go.tz).
Taarifa sahihi za mwenendo wa mvua na tahadhari za hali mbaya ya hewa zinatolewa  na zinapatikana kupitia njia rasmi za utoaji taarifa maalum za kiofisi (official weather statement).
Hivyo taarifa kuhusiana na mvua zinazoendelea imekuwa ikitolewa katika utabiri wa kila siku kupitia vyombo vya habari, mtandao wa kijamii  wa Mamlaka na tovuti ya Mamlaka.
Tunawatakia shughuli njema katika ujenzi wa Taifa letu.
IMETOLEWA NA MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA

Related

MIYEYUSHO KUZIPIGA NA NORFAT OKTOBA 5 MKWAKWANI TANGA

Bondia Francis Miyeyusho kushoto akitunishiana misuli na Emilio Norfat baada ya kusaini mkataba wa kuzipiga Oktoba 5 katika uwanja wa Mkwakwani Tanga mpambano wa raundi nane  katikat...

ALEX MSAMA ATANGAZA VITA NA WEZI WA KAZI ZA WASANII, ASEMA WATASAKWA POPOTE WALIPO

Mkurugenzi wa kampuni ya Msama Promotion ya jijini Dar es salaam Bw. Alex Msama akimwaga furushi lililojaa CD na DVD feki za kazi mbaimbali za wasanii zinazorudufiwa kwa wizi na watu wasiokuwa waa...

TAARIFA YA JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA KWA VYOMBO VYA HABARI TAREHE 01/09/2014

KATIKA TUKIO LA KWANZA: MTU MMOJA ALIYEFAHAMIKA KWA JINA LA FUNUA MAGOKO (35) MKAZI WA ITUMBI ALIUAWA KWA KUPIGWA FIMBO SEHEMU ZA KICHWANI NA WATU WALIOFAHAMIKA KWA MAJINA YA 1. LUGANO GEORGE (3...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904763
item