WANANCHI WAJUMUIKA KWENYE MAZISHI YA SHEIKH ILUNGA JIJINI DAR ES SALAAM JANA

  Maalim Seif akishiriki katika mazishi ya Sheikh wa Ilunga Shekh.Hassan Kapungu yaliofanyika katika makaburi ya Mwinyimkuu Magomeni D...

 Maalim Seif akishiriki katika mazishi ya Sheikh wa Ilunga Shekh.Hassan Kapungu yaliofanyika katika makaburi ya Mwinyimkuu Magomeni Dar es Salaam. akijumuika na Wanancjiji Dar-es-Salaam.

 Wananchi wakishiriki katika mazishi ya Shekh Ilunga  Hasaan Kapungu katika makaburi ya Magomeni Mwinyimkuu jijini Dar-es-Salaam.
Wananchi wakishiriki katika mazishi ya Shekh Ilunga  Hasaan Kapungu katika makaburi ya Magomeni Mwinyimkuu jijini Dar-es-Salaam. (Picha na Salmin Said OMKR)

Na Hassan Hamad (OMKR).

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad, amewaongoza maelfu ya waislamu katika mazishi ya sheikh maarufu wa Mkoa wa Mwanza na mwanaharakati wa dini ya Kiislamu marehemu sheikh Ilunga Hassan Kapungu.

Sheikh Ilunga amefariki dunia mjini Dar es Salaam na kuzikwa katika makaburi ya Mwinyimkuu Magomeni.

Katika uhai wake sheikh Ilunga Kapungu alikuwa mwanaharakati ambaye mara nyingi alikuwa akiendesha mihadhara ya wazi ya dini ya Kiislamu, ambapo mwishoni mwa mwaka 2013 alikamatwa kwa tuhuma za uchochezi mkoani Tabora na baadaye kuachiwa huru.

Kwa mujibu wa taarifa za kimtandao, kabla ya kukamatwa kwake na kuachiwa huru Disemba mwaka 2013, marehemu sheikh Ilunga alikwenda nchini India kwa matibabu baada ya kusumbuliwa na matatizo ya figo pamoja na sukari.

Akizungumza katika mazishi hayo  sheikh Basaleh wa Dar es Salaam, amesema marehemu sheikh Ilunga alikuwa mwanaharakati imara na ni mfano mzuri wa kuigwa katika harakati za dini ya Kiislamu.

Mazishi yake yameweka historia baada ya maelfu ya waislamu kujitokeza kushiriki kwao, hali iliyopelekea mchanga wa kaburi lake kufukiwa kwa mikono badala ya kutumia mapauro na majembe kama ilivyozoeleka.

Masheikh kutoka Mikoa mbali mbali ya Tanzania wameshiriki mazishi hayo akiwemo sheikh Kishki.

Related

ZANZIBAR YATIA SAINI NA KAMPUNI YA SHELL KATIKA KUSHIRIKI KUENDELEZA SEKTA YA MAFUTA NA GESI

Na Said Ameir, Uholanzi Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Kampuni ya Mafuta ya Shell ya Uholanzi zimetia saini Makubaliano ya Ushirikiano katika kuendeleza sekta ya mafuta na gesi. Makubali...

WATU 5 WAJERUHIWA HAI

Watu watano wamejeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari aina ya Hiace na gari dogo eneo la KIA wilayani Hai usiku huu. majeruhi wako hospitali ya wilaya kwa matibabu zaidi, polisi wamethibitisha kuto...

TRAFIKI FEKI KUMBE NI MFUNGWA ALIYETOROKA JELA

  Na Mwandishi WetuMAZITO tena yameibuka kuhusu yule trafiki feki James Hussein, mkazi wa Kimara Matangini, jijini Dar es Salaam ambaye yuko  Gereza la Segerea, Dar akikabiliwa na kes...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item