BAADA YA TIMU YA TAIFA YA ITALIA KUTOLEWA KOMBE LA DUNIA, CESARE PRANDELLI AJIUZULU

Cesare Prandelli Kocha Cesare Prandelli ametangaza kubwaga manyanga baada ya Azzuri kutolewa kwenye mashindano ya Kombe la dunia yan...

Cesare Prandelli

Kocha Cesare Prandelli ametangaza kubwaga manyanga baada ya Azzuri kutolewa kwenye mashindano ya Kombe la dunia yanayoendelea nchini Brazil.

Italia iliondolewa baada ya kufungwa kwa goli 1-0 na Uruguay katika mechi ya mwisho ya makundi. Baada ya mchezo Prandelli akiwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari alitangaza kujiuzulu kuifundisha timu hiyo.“Nilichagua mfumo fulani wa ukufunzi na ndio sababu ninajiuzulu, kwa sababu haukufanya kazi,” alisema.

Aliongezea: “Kuna jambo ambalo limebadilika tangu nilipotia saini mkataba mpya. Sijui kwanini lakini sina haja ya kutafuta sababu .”
Kocha huyo aliingia mkataba mpya na Italy Mei mwaka huu ambao ungemfanya aendelee kuifundisha Italy hadi baada ya mashindano ya kuwania ubingwa wa Euro ya mwaka wa 2016.
Prandeli amechukua hatua hii baada ya kujiuzulu kwa rais wa shirikisho la kandanda la Italia Giancarlo Abete.
“Nilizungumza na rais wa shirikisho na naibu wa rais Demetrio Albertini na nikawapa barua ya kujiuzulu kwangu. Ni jambo lisilobadilika,
Wakati huo huo FIFA imeanza kuchunguza tukio la mshambuliaji wa Uruguay Luis Suarez la tuhuma za kumng'ata begani beki wa Italia Giorgio Chiellini.

Related

SHEHENA YA KEMIKALI YAZUA TAHARUKI, NI BAADA YA TRENI YA MIZGO KUPINDUKA KIJIJI CHA KIFURU MKOANI PWANI.

Mafundi wa Mamlaka ya Reli ya Tanzania na Zambia (TAZARA) wakikarabati kipande cha reli mwishoni mwa wiki kilichoharibika baada ya treni ya mizigo iliyokuwa imebeba shehena ya madini ya salfa kuan...

WATU 27 WAMEOKOLEWA AJALI YA MTUMBWI ZIWA TANGANYIKA, 6 WAMEFARIKI

Na Mwajabu Hoza Kigoma. WATU sita wamekufa 27 wameokolewa na wengine 11 kulazwa katika hospitali ya rufaa maweni iliyopo Manispaa ya Kigoma Ujiji mkoani Kigoma baada ya boti walilokuwa wakisafi...

DKT JAKAYA MRISHO KIKWETE APOKEA RASIMU YA MWISHO YA KATIBA INAYOPENDE​KEZWA UWANJA WA JAMHURI DODOMA

  Mwenyekiti wa Bunge maalum la katiba Mhe.Samuel Sitta akikabidhi rasimu ya katiba inayopendekezwa kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Jakaya Mrisho kikwete na Rais wa Serik...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904977
item