BAADA YA TIMU YA TAIFA YA ITALIA KUTOLEWA KOMBE LA DUNIA, CESARE PRANDELLI AJIUZULU

Cesare Prandelli Kocha Cesare Prandelli ametangaza kubwaga manyanga baada ya Azzuri kutolewa kwenye mashindano ya Kombe la dunia yan...

Cesare Prandelli

Kocha Cesare Prandelli ametangaza kubwaga manyanga baada ya Azzuri kutolewa kwenye mashindano ya Kombe la dunia yanayoendelea nchini Brazil.

Italia iliondolewa baada ya kufungwa kwa goli 1-0 na Uruguay katika mechi ya mwisho ya makundi. Baada ya mchezo Prandelli akiwa kwenye mkutano wa waandishi wa habari alitangaza kujiuzulu kuifundisha timu hiyo.“Nilichagua mfumo fulani wa ukufunzi na ndio sababu ninajiuzulu, kwa sababu haukufanya kazi,” alisema.

Aliongezea: “Kuna jambo ambalo limebadilika tangu nilipotia saini mkataba mpya. Sijui kwanini lakini sina haja ya kutafuta sababu .”
Kocha huyo aliingia mkataba mpya na Italy Mei mwaka huu ambao ungemfanya aendelee kuifundisha Italy hadi baada ya mashindano ya kuwania ubingwa wa Euro ya mwaka wa 2016.
Prandeli amechukua hatua hii baada ya kujiuzulu kwa rais wa shirikisho la kandanda la Italia Giancarlo Abete.
“Nilizungumza na rais wa shirikisho na naibu wa rais Demetrio Albertini na nikawapa barua ya kujiuzulu kwangu. Ni jambo lisilobadilika,
Wakati huo huo FIFA imeanza kuchunguza tukio la mshambuliaji wa Uruguay Luis Suarez la tuhuma za kumng'ata begani beki wa Italia Giorgio Chiellini.

Related

OTHER NEWS 9202278863896039136

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item