WAMBURA RUKSA KUGOMBEA URAIS SIMBA

  Mgombea wa nafasi ya urais klabuni hapo, Michael Wambura RASMI Kamati ya rufani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imemrej...

 Mgombea wa nafasi ya urais klabuni hapo, Michael Wambura



RASMI Kamati ya rufani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imemrejesha Mgombea wa Urais wa Simba SC, Michael Richard Wambura kwenye mbio za kuwania uongozi wa Wekundu wa Msimbazi.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Wakili Julius Lugaziya amewaambia Waandishi wa Habari mchana wa leo (jana) ofisi za TFF katikati ya Jiji la Dar es Salaam, kwamba Wambura amerejeshwa baada ya kikao chao kilichodumu kwa siku mbili.

Baada ya mlolongo mrefu tangu juzi Saa 5:00 asubuhi hoteli ya Courtyad, Upanga, Dar es Salaam hadi jioni ya jana (juzi), Wajumbe wa Kamati hiyo waliamua kupiga kura kuamua na Wambura akapata kura tatu kati ya tano za kumkubalia aendelee na mbio za Urais Simba SC.
Ikumbukwe Wambura alikata rufaa TFF akipinga uamuzi wa Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC kumuengua katika kinyang’anyiro cha kuwania urais katika uchaguzi wa klabu hiyo unaotarajiwa kufanyika mwishoni mwa mwezi huu.

Kamati ya Uchaguzi ya Simba SC chini ya Mwenyekiti Wakili Dk. Damas Ndumbaro ilimuengua Wambura kwa sababu alikiuka Katiba ya klabu hiyo, TFF na FIFA kwa kuipeleka klabu hiyo mahakamani.

Related

Balozi Juma Mwapachu awa Mwenyekiti Bodi ya Wakurugenzi Airtel Tanzania

     Balozi Juma Volter Mwapachu   KAMPUNI tanzu ya Bharti Airtel inayoongoza katika utoaji wa huduma za simu za mkononi ikifanyakazi katika nchi 20 Asia na Afrika, le...

NAULI MPYA ZA USAFIRI WA TRENI KWENDA MWANZA, TABORA, DODOMA NA KIGOMA KUANZIA APRILI 01, 2015

NAULI ZA TRENI YA DELUXE KUANZIA APRILI 01, 2015 DAR - KIGOMA/MWANZA Dar - Dodoma daraja la kawaida: TZS 18,500 Kukaa: TZS 24,700, Kulala: TZS 41,200. Dar - Tabora daraja la kawaida: 25,400, Ku...

ZITTO KABWE NJIA PANDA, CHADEMA WAMFUKUZA

Zitto Kabwe Dar es Salaam. Hali ya kisiasa ya mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe imewekwa njiapanda baada ya Chadema kutangaza kumvua uanachama saa chache baada ya Mahakama Kuu kutupilia...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904758
item