MAJAMBAZI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KIMANZICHANA NA KUUA ASKARI.

Mnamo 11/06/14 huko kituo kidogo cha Kimanzichana Pwani, watu wasiojulikana waliojifanya kuwa ni raia wema waliingia kituo kidogo cha ...

Mnamo 11/06/14 huko kituo kidogo cha Kimanzichana Pwani, watu wasiojulikana waliojifanya kuwa ni raia wema waliingia kituo kidogo cha Polisi Kiman nanzi Chana huku wakikimbia wakiwa na silaha za jadi kiasi cha askari wa zamu kuamini kuwa ni watu wanaohitaji msaada. 
Cha kushangaza watu hao walimvamia askari mwenye silaha ambaye amefahamika kwa jina la JOSEPH NGONYANI na kuanza kumkatakata mapanga na hatimaye kupora silaha SMG ikiwa na risasi 30. Ndipo walipoanza kushambulia kwa risasi askari wengine na kufanikiwa kupora SMG ya pili na risasi 30. Hatimaye watu hao wakapora risasi za akiba 41 na kutoweka kusikojulikana. 
Askari Ngonyani alifariki dunia alipokuwa anapatiwa matibabu kwenye hospitali wilaya ya Mkuranga. Askari mwingine aitwaye VENANCE amejeruhiwa mgongoni kwa risasi ambayo bado imo ndani, na kwenye paja la mguu wa kulia. Mgambo Mariam alijeruhiwa kichwani, shingoni na kuvimba bega kutokana na kupigwa sana mateke na kujeruhiwa mbavuni. 
Kwa mujibu wa mganga Mkuu wa zamu wa Hospitali hiyo aitwaye VERONICA MUSIME, anathibitisha askari huyo kufariki akiwa anapatiwa matibabu hapo Mkuranga wakati wengine wamekimbizwa Muhimbili kwa matibabu ya kina. Kazi ya Mungu haina makosa; vituoni tuwe makini sana na stahili hii ya ujambazi; HESHIMA PEKEE kwa marehemu na majeruhi hawa ni kuwapata watuhumiwa wote na silaha walizoiba bila kuchelewa. Bila kujali mkoa ulipo, taarifa za haraka tunatarajia kupata toka kwako kuhusiana na wahusika wa tukio hili. 
R.I.P Joseph Ngonyani

Related

RATIBA YA ZIARA YA AWAMU YA KWANZA YA UKAWA

TAREHE 14 – 27 MEI 2014. TIMU “A”- KANDA YA KATI 1. Mhe. Mosena Nyambabe (NCCR) – Katibu Mkuu, 2. Mhe. Ashura Mustapha (CUF) – Mjumbe wa Baraza Kuu, 3. John Heche (CHADEMA) – Mwenyekiti wa Vijana ...

WAZIRI MKUU PINDA AZIAGIZA TAKUKURU, MKAGUZI NA MDHIBITI MKUU WA HESABU ZA SERIKALI (CAG) KUICHUNGUZA IPTL

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda Dodoma TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) pamoja na Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) wameagizwa kuchunguza na kujiridhisha kam...

BALOZI WA MALAWI NCHINI TANZANIA AFARIKI DUNIA JIJINI DAR ES SALAAM

Balozi wa Malawi nchini Tanzania Mhe. Flossy Gomile-Chidyaonga  (pichani) amefariki dunia jana jijini Dar es salaam baada ya kuugua kwa muda mfupi. “Ni kwa masikitiko makubwa Wizara ya ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item