TANZANIA KUUNGANA NA JUMUIYA YA KIMATAIFA KUADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA HIFADHI YA TABAKA LA OZONI.

Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, Mhe. Mhandisi Dkt. Binilith Mahenge akiongea na waandishi wa habari kuhusu Maadhi...


Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais - Mazingira, Mhe. Mhandisi Dkt. Binilith Mahenge akiongea na waandishi wa habari kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni linalofanyika leo 16 Septemba, 2014.

DODOMA
Tarehe 16 Septemba, mwaka huu Tanzania inaungana na Jumuiya ya Kimataifa katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Hifadhi ya Tabaka la Ozoni kama ilivyoagizwa na Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika azimio lake la 49/114 la tarehe 19 Desemba, 1994.

Hayo yamesemwa na Waziri wa nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Mhe. Mwandisi Dkt. Binilith Mahenge wakati alipofanya mkutano na waandishi wa habari 15 Septemba, 2014 kwa lengo la kuongelea juu ya Maadhimisho hayo yanayofanyika leo tarehe 16 Septemba mwaka huu.

Mawiri Mahenge ameeleza kuwa tarehe hiyo ni kumbukumbu ya kutiwa saini Mkataba wa Montreal (Montreal Protocol-1987) kuhusu kemikali zinazomonyoa Tabaka la Ozoni kwa kudhibiti utengenezaji na matumizi ya kemikali zinazoharibu Tabaka hilo.

Ameendelea kwa kusema kuwa Mkataba huo umepata mafanikio makubwa ya kupunguza zaidi ya asilimia 98% ambapo ni takribani tani milioni 1.8 ya uzalishaji na matumizi ya kemikali zinazomong’onyoa Tabaka la Hewa ya Ozoni.

“Punguzo hilo limechangia katika juhudi za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwasababu baadhi ya kemikali zinamong’onyoa tabaka la ozoni pia husababisha kuongezeka kwa joto duniani”, alisema Dkt. Mahenge.

Related

MAONI YA MSEMAJI WA KAMBI RASMI YA UPINZANI BUNGENI, WIZARA YA SHERIA NA KATIBA, MHESHIMIWA TUNDU A.M. LISSU KUHUSU MUSWADA WA SHERIA YA MAREKEBISHO YA SHERIA YA MABADILIKO YA KATIBA, YA MWAKA 2013

  (Kanuni ya 86(6) ya Kanuni za Kudumu za Bunge, 2013) UTANGULIZI Mheshimiwa Spika, Huu ni Muswada wa marekebisho ya pili ya Sheria ya Mabadiliko ya Katiba, Sura ya 83 ya Sheria z...

BUNGE NA SONGOMBINGO LAKE KATIKA PICHA, HALI INATISHA

SEHEMU NAMBA MOJA. Hapa askari wa bunge wakipambana na mhe Joseph Mbilinyi huko mhe akiwa ameshika mkono wa kipaza sauti kufuatia kutoelewana ndani ya ukumbi wa bunge jana WATU AAAH, MSHANG...

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Abdulrahaman Kinana septemba 10 anatarajiwa kuanza ziara ya kawaida katika mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara. Ziara hiyo itaanzia katika mkoa wa ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904775
item