Shirika la "Tanzania Sisi kwa Sisi Foundation (TSSF)" LAFUTIWA USAJILI kwa tuhuma ya kujihusisha na kuhamasisha ushoga nchini

  WIZARA ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imelifutia usajili Shirika la Tanzania Sisi kwa Sisi Foundation (TSSF), kwa tuhuma ...

 
WIZARA ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto imelifutia usajili Shirika la Tanzania Sisi kwa Sisi Foundation (TSSF), kwa tuhuma ya kujihusisha na kuhamasisha ushoga nchini.
Taarifa kwa umma iliyotolewa na Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali wizarani, ilieleza kuwa shirika hilo limefutiwa usajili kuanzia Aprili 4, mwaka huu.
Ilieleza kuwa kufungiwa huko, kunatokana na kukiuka masharti ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2002 na sheria mbalimbali za nchi.

“Taarifa inatolewa kwa umma kuwa shirika la Tanzania Sisi kwa Sisi Foundation (TSSF) lililosajiliwa chini ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali mwaka 2011, limefutiwa usajili kuanzia tarehe 04.04.2014 kutokana na kukiuka masharti ya Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali ya mwaka 2002 na sheria mbalimbali za nchi.Kwa taarifa hii, utendaji kazi wa shirika hili unasitishwa kwa mujibu wa Sheria ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Namba 24 ya mwaka 2002 na utendaji kazi wake baada ya taarifa hii, utakuwa ni kinyume cha sheria,” ilieleza taarifa hizo ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali.
 
Mmoja wa viongozi wa wizara hiyo, alieleza kuwa shirika hilo limefungiwa kutokana na vitendo vya ushoga, lakini hana taarifa zaidi na kutaka watendaji waulizwe.
 
Baada ya taarifa hiyo, mtu mmoja ambaye namba zake zinaonekana katika mtandao wa kijamii wa shirika hilo, ukielekeza wanaume wanaojihusisha na vitendo vya kishoga kumuandikia taarifa kwa ajili ya semina, alipoulizwa kuhusu taarifa hizo, kwamba wamefutiwa leseni alisema hawana taarifa.
 
Akizungumza na habari leo, mtu huyo aliyesema ofisi zao ziko Ilala jijini Dar es Salaam, aliyekataa kutaja jina lake, alisema hawajapewa barua ya kusitisha huduma zao, hivyo wataendelea na huduma zao mpaka wapewe taarifa.
 
Mtu huyo ambaye awali alijitambulisha kwa jina la Dk John, ambaye namba zake zinaonekana katika maelezo ya taasisi hiyo katika mitandao, alisema hana taarifa zozote na yuko nje ya nchi.
 
Alisema namba hiyo ni kwa ajili ya huduma za wateja. Alisema hajaliona tangazo wala hana taarifa.
 
Hivi karibuni katika mitandao ya jamii, watu kadhaa walililalamikia shirika hilo, lililosajiliwa na serikali kujihusisha kudai haki, wakidai linahamasisha ushoga nchini. Mtandao wa kijamii wa shirika hilo, una tangazo linalowaalika wanaume wanaojihusisha na vitendo hivyo.
 
"Je, wewe ni mwanaume unayejihusisha katika mapenzi ya jinsia moja?TSSF inakualika katika semina fupi, itakayofanyika kesho Ijumaa ya tarehe 21 Februari 2014 kuanzia saa 4 asubuhi.
 
“Mada zitakazoongelewa ni: Magonjwa ya ngono yanayowaathiri kuchu; Namna ya kujilinda na magonjwa hayo, Kujiepusha na magonjwa hayo na tiba. Kwa maelezo ya jinsi ya kuhudhuria tupigie katika 0752648253 au tutumie meseji.

Related

OTHER NEWS 6080768373042899971

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item