MSAJILI WA VYAMA VYA SIASA JOHN TENDWA KUKIFUTA CHADEMA

Msajjili wa vyama vya siasa, John Tendwa Hatimaye msajili wa vyama vya siasa nchini, John Tendwa ameibuka na kusema sasa anaandaa kalam...

Msajjili wa vyama vya siasa, John Tendwa
Hatimaye msajili wa vyama vya siasa nchini, John Tendwa ameibuka na kusema sasa anaandaa kalamu yake kukifuta Chama kikuu cha upinzani nchini CHADEMA.
Katika Taarifa yake kwa vyombo vya habari  Tendwa amesema CHADEMA wanataka kuanzisha kikundi cha mgambo ambacho ni kinyume na sheria, katiba ya nchi na sheria za usajili wa vyama.
Msajili huyo amesema kwamba kama madai ya CHADEMA ni kuanzisha kikundi cha kujilinda dhidi ya Green Guard wa CCM madai hayo hayana msingi wowote kwani kama CHADEMA wana taarifa kwamba Green Guard wanahatarisha amani basi wanapaswa kuripoti suala hilo polisi ili lifanyiwe kazi kwa mujibu wa sheria.
Tendwa amezidi kuonya kwamba uamuzi wake ni wa mwisho na atakapoifuta CHADEMA maamuzi yake hayapingwi popote kisheria.

Source:  Global Publishers

Related

WARAKA ULIOWATOA KINA ZITTO KABWE MADARAKANI NDANI YA CHADEMA HUU HAPA

MKAKATI WA MABADILIKO 2013 UTANGULIZI. Taasisi tunayoizungumzia ilisajiliwa rasmi mwezi January 1993 na tokea wakati huo imeongozwa na wakuu wa taasisi wapatao wawili na aliyepo kwa sasa ...

ZITTO KABWE, SAMSONI MWIGAMBA NA DKT. KITILA MKUMBO WAVULIWA UONGOZI NA KAMATI KUU YA CHADEMA

Kamati kuu ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema imewavua Uongozi Viongozi wake watatu baada ya Kugundua waraka wa Siri uliowahusisha na mpango wa kukipasua Chama vipande vipande. Viongoz...

RAIS KIKWETE AWAPANDISHA VYEO MAKAMISHNA 77 JESHI LA POLISI

Amiri Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo maofisa 77 wa Jeshi la Polisi kutoka Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) kuwa Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP). Taarifa ...


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item