SIMBA YAKABIDHIWA SH MILLIONI 20 KWA AJILI YA MKUTANO MKUU

Meneja wa Kili, George Kavishe akimkabidhi Katibu wa Simba SC, Evodius Mtawala mfano wa hundi ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya Mkuta...

Meneja wa Kili, George Kavishe akimkabidhi Katibu wa Simba SC, Evodius Mtawala mfano wa hundi ya shilingi milioni 20 kwa ajili ya Mkutano Mkuu wa wanachama wa klabu hiyo
Jana KILI imekabidhi hundi ya Sh. Milioni 20 kwa klabu ya Simba SC kwa ajili ya mkutano mkuu wa klabu hiyo utakaofanyika Julai 20, 2013 jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi hundi hiyo Meneja wa Kili, George Kavishe alisema: “Tunakabidhi fedha hizi ikiwa ni mwendelezo kutekeleza majukumu yetu kama mdhamini mkuu wa Simba SC. Kwa kuzingatia hilo tungependa kuona maendeleo ya klabu ya Simba uwanjani na nje ya uwanja. Tunaiunga mkono klabu hii katika mkutano wake mkuu tukiamini kuwa mkutano huu utaimarisha uhusiano uliopo kati ya klabu na wanachama wake kwa kuwapa fursa ya kuhakiki mwelekeo wa klabu yao waipendayo.
Kavishe alieleza zaidi, “Ikiwa na mamilioni ya mashabiki nchini, klabu hii imejengeka kutokana na rekodi nzuri ya mafanikio kwa muda mrefu – na Kili inajivunia kuwa sehemu ya klabu hii. Tunaamini kwamba mbali na wanachama, wapenzi na mashabiki wa Simba kuona timu yao ikishinda lakini pia tunatambua kwamba ni haki yao ya msingi kuwasiliana na klabu na kupata taarifa mbalimbali za mwenendo wa klabu. Kutokana na sababu hizi, sisi kama wadhamini wakuu wa klabu hii tunatoa mchango wa shilingi milioni ishirini ili kuunga mkono jitihada za klabu kuendelea kuwajibika kwa wanachama wake.
“Tunatambua wajibu wetu kama wadhamini wakuu wa Simba katika kutekeleza mkataba wetu, tutaendelea kushirikiana na kufanya kazi kwa pamoja ili kuhakikisha tunalipeleka soka la Tanzania kwenye kilele cha mafanikio."

Related

MLIPUKO KIWANDA CHA MITSHUBISHI JAPAN WAUA WATU 5

Watu watano (5) wamekufa na wengine 17 wamejeruhiwa katika mlipuko uliotokea leo kwenye kiwnda cha Mitsubishi kilichopo km 350 Magharibi mwa Tokyo nchini Japan.

KUTEKWA NA KUTESWA MWENYEKITI WA TEMEKE, MPANGO MZIMA WA KUIHUSISHA CHADEMA HUU HAPA

Jana majira ya saa 3.30 asubuhi, watu wapatao watano ambao ni wanachama wa CHADEMA mamluki wa Timu ya Zitto na CCM, wakiwa eneo moja la ofisi ya umma wakisubiri huduma ya muhimu sana, walipokea...

TAMKO LA CHADEMA KUFUATIA TUKIO LA KUTEKWA, KUTESWA NA KUUMIZWA KWA MWENYEKITI WA CHADEMA WILAYA YA TEMEKE

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa mshtuko taarifa za tukio la kutekwa, kuteswa na kuumizwa kwa Mwenyekiti wa CHADEMA Wilaya ya Temeke, Jos...


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item