Endapo itatokea Mhe. Edward Lowassa akagombea Urais kweli sintompa kura yangu-Kigwangalla

Mbunge wa jimbo la Nzega,Hamis Kigwangalla- Jana nilialikwa na dada yangu Fina wa Mango kwenye show yake adhimu ya Makutano na...


Mbunge wa jimbo la Nzega,Hamis Kigwangalla- Jana nilialikwa na dada yangu Fina wa Mango kwenye show yake adhimu ya Makutano na Fina Mango. Nianze kwa kumshukuru dada Fina na timu yake kwa kazi nzuri wanayofanya. 

Nimshukuru pia Ndg. Uswege Mwaipyana (my Twitter friend) kwa kupendekeza nialikwe na Fina kwenye show, baada ya yeye (Uswege) kufuatilia ile iliyopita Jumamosi iliyotangulia na kuona ingependeza kama nami ningealikwa. 

Niliongelea mambo mengi ikiwemo historia yangu ya utoto na nilivyougua kwashiakor na marasmus na kuponea chupuchupu kufariki dunia kijijini Goweko, Mlimani kwa babu yangu, elimu yangu na uzoefu wangu kwenye uongozi kwenye taasisi mbalimbali nilizopitia. Niliongelea mapinduzi ya kilimo cha Pamba na Alizeti Nzega ambayo ninayaongoza na pia ndoto zangu za Urais, utendaji wa Rais Kikwete na pia hatma ya Taifa letu kwenye mchakato wa kumpata Rais mpya 2015.

 Dada Fina Mango aliniuliza swali moja lililohusisha Urais 2015 na Mhe. Edward Ngoyai Lowassa (Mb.) ambaye anatajwa tajwa kuwa huenda akawemo among presidential contenders watarajiwa. Majibu yangu yote yalijikita, kama ilivyo kawaida yangu, kwenye ukweli na kwenye tafsiri sahihi ya kimantiki inayotokana na uelewa na utashi wangu. 

Ni kweli nilisema kuwa endapo itatokea Mhe. Edward Lowassa akagombea Urais kweli sintompa kura yangu, sikutafuna maneno, na wala sina chuki ama uadui naye, na nilisema ametenda mengi mazuri na nilisifia ujasiri na umahiri wake kabla ya suala la Richmond, naam kabla ya Richmond saga, niligusia dedication yake, lakini nilihitimisha kwa kusema kuwa kwa zama hizi siwezi kumuunga mkono. Alipofikia panatosha. Naam, panatosha. Kwa kuwa kuna script ya nilichokiongea, acha nikiweke wazi hapa ili wenye kupenda kufuatilia suala hili wajisikilizie wenyewe.

Related

HOTUBA YA WAZIRI WA FEDHA, MHESHIMIWA SAADA MKUYA SALUM (MB) AKIWASILISHA BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA YA FEDHA KWA MWAKA 2014/15.

UTANGULIZI 1. Mheshimiwa Spika, kufuatiataarif ailiyowasilishwa hapa Bungeni na Mwenyekiti wa Kamatiya Kudumu ya Bunge ya Uchumi, Viwanda naBiashara, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lakoTukufu li...

WAMBURA RUKSA KUGOMBEA URAIS SIMBA

 Mgombea wa nafasi ya urais klabuni hapo, Michael Wambura RASMI Kamati ya rufani ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) imemrejesha Mgombea wa Urais wa Simba SC, Michael Richard Wambur...

MAJAMBAZI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KIMANZICHANA NA KUUA ASKARI.

Mnamo 11/06/14 huko kituo kidogo cha Kimanzichana Pwani, watu wasiojulikana waliojifanya kuwa ni raia wema waliingia kituo kidogo cha Polisi Kiman nanzi Chana huku wakikimbia wakiwa na silaha za...


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904776
item