SHERIA BARAZA LA VIJANA LA TAIFA, MNYIKA AWASILISHA MUSWADA BINAFSI

Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, amewasilisha kwa Katibu wa Bunge taarifa ya muswada binafsi wa Sheria ya Baraza la Vijana la T...

Mbunge wa Ubungo (Chadema), John Mnyika, amewasilisha kwa Katibu wa Bunge taarifa ya muswada binafsi wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa.
 
Kwa mujibu wa Mnyika, taarifa hiyo inaeleza madhumuni na sababu za muswada. Mbali na taarifa hiyo, Mnyika pia amewasilisha nakala ya muswada husika na hivyo kukidhi matakwa ya kanuni ya Bunge ya 81 (2).
 
Mnyika alisema baada ya kuwasilisha vitu hivyo, hatua inayopaswa kufuatwa ni Katibu wa Bunge kutumia mamlaka yake kwa mujibu wa kanuni ya Bunge ya 81 (3), kutangaza muswada huo kwenye Gazeti la Serikali ili usomwe kwa mara ya kwanza kabla ya kumalizika kwa Mkutano wa Bunge unaoendelea.
 
Alisema amechukua hatua hiyo baada ya ratiba ya mkutano wa sasa wa Bunge kuonyesha kwamba Muswada wa Sheria ya Baraza la Vijana la Taifa haupo katika orodha ya miswada ambayo serikali inakusudia kuiwasilisha, kinyume cha ahadi za mara kwa mara zilizotolewa za kuuwasilisha.
 
Kwa mujibu wa Mnyika, alitarajia kwamba tarehe ya juzi ambayo ilikuwa ni Siku ya Vijana wa Afrika, serikali ingetumia nafasi hiyo kutoa taarifa ya utekelezaji wa mkataba wa vijana wa Afrika ambao uliridhiwa na Bunge mwaka 2011.
 
Alisema kifungu cha 11 cha mkataba huo ambao Rais Jakaya Kikwete alishiriki katika mkutano wa kuuandaa mwaka 2006, kinataka nchi wanachama wa Umoja wa Afrika (AU) kuhakikisha ushiriki wa vijana kwa pamoja na mambo mengine kuwezesha kuundwa kwa mabaraza ya vijana.
 
Alisema mkataba huo unaelekeza kwamba mabaraza yaundwe kuanzia kwenye ngazi ya mitaa mpaka taifa kuwezesha vijana kushiriki katika maamuzi na kutekeleza kikamilifu kazi mbalimbali za maendeleo.
 
“Katika muktadha huo sehemu ya nne ya muswada huo, hususan vifungu vyake vya 27 na 28 vimewekwa utaratibu wa kuundwa kwa majukwaa (mabaraza) ya vijana kwenye ngazi za vijiji/mitaa, kata na wilaya,” alisema Mnyika.
 
Pia alisema sehemu ya sita ya muswada ina vifungu vinavyohusu Mfuko wa Maendeleo ya Vijana hususan kifungu cha 31 (1) kinachoeleza kwamba mfuko huo utaundwa kwa ajili ya kuliwezesha baraza kutekeleza miradi ya vijana kwa ajili ya maendeleo ya vijana. 

Vilevile, kuwezesha utekelezaji wa mipango ya baraza na kugharimia shughuli za baraza hilo.

Related

OTHER NEWS 8475162122581061687

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item