DKT. ASHA - ROSE MIGIRO AAPISHWA BUNGENI LEO

MBUNGE wa kuteuliwa na Rais,  Dk. Asha-Rose Migiro, leo saa 3 asubuhi, ameapishwa kuwa mbunge wa Bunge la Tanzania. Akizungumza nje ya ...

MBUNGE wa kuteuliwa na Rais,  Dk. Asha-Rose Migiro, leo saa 3 asubuhi, ameapishwa kuwa mbunge wa Bunge la Tanzania.

Akizungumza nje ya viwanja vya Bunge, baada ya kuaspishwa, na Spika wa Bunge Anna Makinda,  Dk. Asha-Rose ameahidi utumishi wenye uadilifu, uaminifu na wa kujituma.

Alisema  ubunge ni uwakilishi uwe wa kuteuliwa, kupitia viti maalum au majimbo na kwamba nafasi hiyo aliyopewa sio ya kwake binafsi bali ni heshima kwa wanawake wote nchini.

"Unapopewa fursa kama hiyo sio yako binafsi bali ni heshima ya wanawake wote kwa sababu nimeongeza idadi ya waliopo bungeni’’

“Hivyo ni nafasi nyingine kuwa wanawake tunawajibu na tunapopata fursa basi tuna kila sababu ya kutumikia umma na Nchi yetu kwa moyo wote na kwa nguvu zote,"alisema Dk. Migiro.

Kwa  mara nyingine Dk. Migiro alimshukuru  Rais Dk. Jakaya  Kikwete  kwa uteuzi wake kwake kwa kuwa umempa  heshima na fursa nyingine ya kutumikia  Taifa.

"katika maisha mtu anaweza akafanya kazi yoyote na kazi yoyote ina thamani lakini nafikiria kazi ya kutumikia umma ni heshima ya pekee kwa sababu kama utaweza kufanya shughuli kwa ufanisi basi matokeo yake yanasambaa kwa watu wengi zaidi,"aliongeza Dk. Migiro.

Related

KITETO YAPATA REKODI MBAYA YA MAUAJI BAINA YA WAKULIMA NA WAFUGAJI

Majeruhi wa mapigano hayo Pikipiki ikiwa imeteketezwa Na Mohamed Hamad WILAYA ya Kiteto imeingia kwenye orodha ya maeneo yanayotisha kwa mauaji ya kinyama baada ya wakulima kuuawa mara ...

MAKAMBA AJIPIGIA DEBE LA URAIS KIAINA

Naibu waziri wa Sayansi na Teknologia , January Makamba Katika kile kinachoonekana kama kujipigia debe katika kinyang’anyiro cha urais katika Uchaguzi Mkuu wa 2015, Naibu Waziri wa Mawasiliano,...

MTANZANIA JACK CLIFF AKAMATWA NA MADAWWA YA KULEVYA HUKO MACAU

Jackie akiwa amewekwa mbele ya waandishi wa habari na mzigo wake wote aliokuwa ameumeza..... Waandishi wa habari wakifanya yao Madawa aliyokuwa amemeza Jack Jack Cliff aliyekamatwa n...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item