BOTI YA KILIMANJARO MALI YA AZAM MARINE YAPATA AJALI IKITOKEA PEMBA, MAITI 5 ZAPATIKANA

Boti ya Kampuni ya Azam Marine ya Kilimanjaro  ikitokea Pemba asubuhi ya leo ikiwa na abiria karibu 320 imepata misukosuko ya hali ya...



Boti ya Kampuni ya Azam Marine ya Kilimanjaro  ikitokea Pemba asubuhi ya leo ikiwa na abiria karibu 320 imepata misukosuko ya hali ya upepo na mawimbi na kusababisha baadhi ya abiria waliokuwa wamekaa sehemu ya abiria ya mbele ya boti hiyo na kutumbukia baharini, kutoka na upepo huo.
Ajali hiyo imetokea katika mkondo wa nungwi na baadhi ya abiria wa boti hiyo kuingia baharini kutokana na mawimbi na upepouliokuwa ukivuma katika majira ya asubuhi ya leo na hali ya bahari kuchafuka.
Ikiwa katika safari zake za kawaidi ikitokea Pemba na kuelekea Unguja ilipata dosari kutokana na upepo na mawimbi katika maeneo ya Nungwi.
Juhudi za Wananchi na Vyombo husika kuchukua juhudi za uokoaji wa abiria hao na kufanikiwa kuwapata Wananchi watatu wakiwa hai na miili ya watu 5 kupatikana mpaka sasa.
.
Mpaka sasa kwa taarifa iliopatika jumla ya abiria 4 wameokolewa na kupatikana maiti 5,na zoezi la uokowaji linaendele kufanyika katika eneo la tukio  la bahari ya Nungwi. 

Maiti zilizopatika katika zoezi hili ni 5, na mbili ni za Wanawake na tatu za Wanaume, na zoezi hilo limesitishwa hadi kesho.asubuhi.
Leo katika majira ya asubuhi hali ya bahari ilikuwa na mawimbi na upepo mkali

Related

OTHER NEWS 7105651208843566084

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item