DKT. SHEIN ZIARANI NCHINI INDIA

STATE HOUSE ZANZIBAR OFFICE OF THE PRESS SECRETARY PRESS RELEASE     Zanzibar                                                   ...

STATE HOUSE ZANZIBAR
OFFICE OF THE PRESS SECRETARY
PRESS RELEASE
    Zanzibar                                                                    31 Januari, 2014
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Ali Mohamed Shein anaondoka nchini leo kuanza ziara ya siku tisa nchini India kufuatia mwaliko wa Makamu wa Rais wa nchi hiyo Bwana Mohammad Hamid Ansari.
 
Akiwa nchini humo Dk. Shein anatarajiwa kukutana na viongozi wa nchi hiyo na jumuiya za wafanyabiashara kwa lengo la kukuza uhusiano kati ya Tanzania na India pamoja na kuhimiza ushirikiano kati ya Zanzibar na India katika nyanja za uchumi, biashara, uwekezaji, afya, kilimo na elimu.
 
Katika ziara hiyo mbali na Mke wake Mama Mwanamwema, Dk. Shein amefuatana na Waziri wa Fedha Omar Yusuf Mzee, Waziri wa Uwezeshaji, Ustawi wa Jamii, Vijana, Wanawake na Watoto Bibi Zainab Omar Mohamed, Waziri wa Biashara na Viwanda na Masoko Nassor Ahmed Marzui na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Dk. Mahadhi Juma Maalim.
 
Wengine katika msafara huo ni Katibu Mkuu Wizara ya Afya Mohamed Saleh Jidawi na Katibu Mkuu Kilimo na Maliasili Affan Othman Maalim, Mshauri wa Rais Ushirikiano wa Kimataifa, Uwekezaji na Uchumi Balozi Mohamed Ramia na Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Uwekezaji Zanzibar –ZIPA Salum Khamis Nassor.
Akiwa nchini India Jumapili tarehe 2 Februari, 2014 atatembelea Chuo cha Barefoot kilichoko Tilonia ambako Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inatarajiwa kusaini makubaliano ya ushirikiano na chuo hicho ambacho kimejiegemeza katika kuwajengea uwezo kiuchumi, kijamii na kielimu wanawake wazee na wajane waishio vijijini ili kuinua kiwango chao cha maisha.
 
Siku inayofuata tarehe 3 Februari, 2014 mapema asubuhi atazuru kumbukumbu ya Mahatma Ghandhi ambako ataweka shada la maua na baadae atafanya mazungumzo na Mwenyeji wake Makamu wa Rais.
Baadae mchana siku hiyo atafanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa India Bwana Manmohan Singh, ataonana na Waziri anayeshughulikia Diaspora na Waziri wa Afya na Familia wa nchi hiyo. Jioni atakutana na watanzania wanaioshi Delhi na baadae usiku atahudhuria chakula cha usiku kilichoandaliwa kwa heshma yake na mwenyeji wake Makamu wa Rais wa India.
 
Tarehe 4 Februari, 2014 atatembelea kituo cha utafiti wa mazao ya kilimo, atakutana na Jumuiya ya Wafanyabiashara na kuondoa kwenda mji wa Hyderabad ambako siku inayofuata atakutana na Mwenyekiti wa hospiltali za Appolo na kusaidia Makubaliano ya Ushirikiano.
 
Dk. Shein siku hiyo atakutana pia na Baraza la Biashara ya Madawa Nchi za Nje la India na baadae atapata fursa ya kutembelea kiwanda cha madawa ambapo baadae atasafiri hadi mji wa Bangalore ambako siku ya Alhamisi tarehe 6 Februari, 2014 atatembelea hospitali ya Manipal na kutia saini makubalino ya ushirikiano na hospitali hiyo na baadae kuondoka kwenda Mumbai.
Akiwa Mumbai tarehe 7 Februari, 2014 Dk. Shein atatembelea Kampuni ya kutengeneza matrekta ya Mahindra na baadae jioni atakutana na makampuni ya biashara ya utalii na wakala wa safari za kitalii.
Jumamosi tarehe 8 Februari, 2014 Rais na ujumbe wake utatembelea kiwanda cha kusindika viungo (spices).
Rais wa Zanzibar naMwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi na ujumbe wake utaondoka India Jumapili tarehe 9 Februari, 2014 kurejea nyumbani.
 
Postal Address: 2422 Tel.+255 776 613 015, Fax: 024 2231822  

Related

OTHER NEWS 1440305883069501218

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item