GRACE MVANDA KUWANIA UBUNGE JIMBO LA KALENGA IRINGA

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimempitisha Grace Tendeya Mvanda, kuwa mgombea wake katika kinyang’anyiro c...

KAMATI Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimempitisha Grace Tendeya Mvanda, kuwa mgombea wake katika kinyang’anyiro cha ubunge katika jimbo la Kalenga, mkoani Iringa.

Grace Mvanda alikuwa mtu wa pili katika kinyang’anyiro cha kura za maoni jimboni humo. Aliyeshika nafasi ya kwanza alikuwa ni Lucas Sinkala Mwenda (31) ambaye Kamati Kuu haikupitisha jina lake.

Mwenda ni mhitimu wa Shahada ya Kwanza ya Sheria na sasa anataka kujiunga na Mafunzo ya Sheria kwa vitendo.

Uchaguzi mdogo wa jimbo la Kalenga umepangwa kufanyika 16 Machi 2014. Uchaguzi huu unatokana na aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo, Dk. William Mgimwa kufariki dunia miezi miwili iliyopita nchini Afrika Kusini.

Taarifa za ndani ya kikao zinasema, Kamati Kuu ilijadili kwa kina majina ya wagombea wote wa nafasi hiyo; huku wajumbe wakipata nafasi ya kuwahoji kila mgombea aliyekuwa anatafuta nafasi ya kupeperusha bendera ya chama.

Hatimaye Grace kwa kutumia ripoti za interejensia ya chama na vigezo vingine, aliteuliwa kuwakilisha chama katika kinyang’anyiro hicho.

Miongoni mwa vigezo vilivyotumika, ni kwamba mwanamama huyo aliwahi kugombea ubunge katika jimbo hilo mwaka 2005 kupitia chama cha Jahazi Asilia alishindwa.

Lakini alishika nafasi ya pili nyuma ya mgombea wa CCM. Taarifa zinasema, pamoja na kwamba JAHAZI Asilia hakikuwapo jimboni humo na mkoa wa Iringa kwa ujumla, lakini alifanikiwa kujinyakulia kura 13,500.

“Hii inaonyesha mgombea huyo anakubalika,” anaeleza Tundu Lissu, Mwanasheria mkuu wa chama hicho.

Lucas Sinkala Mwenda, alikubaliana kwa moyo mmoja na maamuzi ya Kamati na ameahidi kutoa ushirikiano kwa mgombea na kukisaidia chama chake kushinda.

Related

MAGUFULI: NITABORESHA MASLAHI YA VYOMBO VYA ULINZI NA USALAMA

MGOMBEA urais kwa teketi ya CCM, Dk.John Magufuli akifafanua jambo kwa msisitizo huku akibainisha kuwa iwapo atachaguliwa kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu, basi Serikali yake itahakikisha inaboresha ...

TASWIRA MBALIMBALI CUF WALIPOZINDUA RASMI KAMPENI ZA URAIS ZANZIBAR

 Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, akisalimiana na Mgombea Urais wa Ukawa wa Zanzibar kupitia Chama cha Wananchi CUF,...

Tume za Uchaguzi Afrika Mashariki zatakiwa kutoa ushirikiano na NEC/ZEC kuelekea uchaguzi Mkuu Oktoba

Tume za Uchaguzi katika Jumuia ya Africa Mashariki zimetakiwa kushirikiana na kutoa ushirikiano kwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) na Tume ya Uchaguzi Zanziba (ZEC) katika kipindi hiki ku...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904762
item