UTALII UNAENDELEA DODOMA, SOMA HAPA ALICHOSEMA JULIUS MTATIRO KUHUSU BUNGE LA KATIBA

Ifikapo ijumaa tarehe 28/02/2014 inategemewa bunge la katiba litajadili na kuidhinisha rasimu ya kanuni za bunge maalum. Ijumaa tareh...


Ifikapo ijumaa tarehe 28/02/2014 inategemewa bunge la katiba litajadili na kuidhinisha rasimu ya kanuni za bunge maalum.
Ijumaa tarehe 28 tayari wajumbe 639 tutakuwa tumelipwa jumla ya shilingi 300,000 x siku 12 x wajumbe 639 = 2,300,400,000/-(bilioni mbili milioni mia tatu na laki nne) au (milioni elfu mbili na mia tatu na laki nne).

La ajabu kuliko yote ni kuwa, wiki mbili zinakatika bila jambo lolote la maana kufanyika. Kambi za urais ndani ya CCM(Presidential Camps) zinapambana kufa na kupona kuhakikisha kambi mojawapo inatoa mwenyekiti wa bunge la katiba.

Kwa utafiti mdogo nilioufanya, ukamilishaji wa kanuni unapigwa danadana ili uchelewe kukamilika kutoa fursa kwa kambi iliyozidiwa kete ili wajipange katika kuusaka uenyekiti wa bunge la katiba.

Kambi ambayo inapigiwq chapuo na CCM ni ile ya Edward Lowassa ambayo mgombea uenyekiti wake ni mhe. Andrew Chenge.

Wakati CCM na Lowassa wanampigania kwa nguvu zote, upande wa pili yupo Samwel Sitta ambaye naye amejizatiti na amewagawa wabunge wa CCM na kuwafanya nusu wamuunge mkono Chenge(kwa kufuata msimamo wa chama) huku nusu wakimuunga mkono Samwel Sitta kutokana na utashi wao kwa kuzingatia rekodi walau ya kuridhisha aliyonayo hasa alipowahi kuwa spika wa bunge.

Rais Kikwete aliwahi kuahidi kuuacha mchakato wa katiba uwe huru, iweje tena leo chama chake kishinikize kwa nguvu nani awe mwenyekiti wa bunge la katiba? Na akishakuwa huyo wanayemtaka pana malengo kuwa aje kusimamia katiba ya watanzania au ya CCM?

Kwa vyovyote vile iwavyo, makundi ya urais ndani ya CCM yataliyumbisha sana bunge la katiba, "mark time" zitapigwa kila siku ili kambi inayopaswa kushinda ijipange, wajumbe tunaendelea kulipwa shilingi milioni 200 kwa ujumla kila kukicha ili kusubiri vita ya mafahali iishe.

Panahitajika mbinyo wa wananchi na sisi tuliomo humu bungeni kuwawakilisha wananchi, haiwezekani ati mchakato huru wa katiba ugeuzwe kuwa mapambano ya kambi za urais. Hili halikubaliki, siku ya ijumaa ikiwa wataleta DELAYS zao tutamweleza KIFICHO na wenzie kuwa tumechoshwa na KUKALISHWA DODOMA na kulipwa posho ambazo ni kodi za wananchi bila kazi.

Kila siku tunawaeleza wanaoyumbisha nchi hii ni CCM, pana watu wanatukejeli, nchi itamalizwa hii and "no body in power cares".

Related

BREAKING NEWS!!!!!!! MOTO WATEKETEZA JENGO LA JANCO MOTEL JIJINI MBEYA USIKU HUU

Moto mkali umezuka katika jengo la Janco Motel lililopo Forest Mpya, Mbeya usiku huu. Hadi sasa Zimamoto hawajafanikiwa kuudhibiti, jengo linateketea. Habari zaidi zitafuata.

TASWIRA YA MBALIMBALI NYUMBANI KWA MAREHEMU DR MGIMWA ALIPOZALIWA

 Hapa  ndipo  nyumbani  alipozaliwa na alipokuwa akiishi  aliyekuwa  waziri  wa fedha na mbunge wa  jimbo la Kalenga Dr Wiliam Mgimwa na ndipo atazikwa h...

MENO YA TEMBO 81 YAKAMATWA BANDARI YA DAR ES SALAAM

Watu wawili wanashikiliwa na polisi nchini Tanzania baada ya kukamatwa na shehena ya meno ya tembo katika bandari ya Dar es Salaam, waliyokuwa wakisafirisha kiharamu maafisa wa nchi hiyo wam...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904809
item