RAIS KIKWETE AONGOZA WATANZANIA KUMBUKUMBU YA MIAKA 30 YA KIFO CHA SOKOINE

Rais Jakaya Kikwete leo ameongozi taifa katika maadhimisho ya miaka 30 ya kifo cha Waziri Mkuu wa zamani Edward Moringe Sokoin...

Rais Jakaya Kikwete leo ameongozi taifa katika maadhimisho ya miaka 30 ya kifo cha Waziri Mkuu wa zamani Edward Moringe Sokoine katika maadhimisho yaliyofanyika nyumbani kwa marehemu Monduli Juu.
Pichani juu Rais Jakaya Kikwete akiweka shada la maua katika kaburi la aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania hayati Edward Moringe Sokoine wakati wa kumbukumbu ya miaka 30 tangu kifo chake.
 Rais Mstaafu, Benjamini Mkapa akiweka shada la maua
  Waziri Mkuu Mstaafu na Mbunge wa Monduli, Edward Lowasa akiweka shada la maua katika Kaburi la marehemu, Edward Moringe Sokoine.
 Spika wa Bunge Anne Makinda akiweka shada la maua.
Mjumbe wa Bunge la Katiba Paul Kimiti akiweka shada la maua kwaniaba ya wajumbe wenzake.
 Rais Kikwete, akiwa katikati ya wajane wa waziri Mkuu wa Zamani Edward Moringe Sokoine wakati wa kumbukumbu ya Kiongozi huyo wa zamani wa Tanzania. Wengine kutokla kushoto ni Mjane wa baba wa Taifa, mama Maria Nyerere, Rais Mstaafu Benjamin Mkapa, Spika wa Bunge, Anne Makinda namotto wa Marehemu sokoine Ndugu Joseph Sokoine.
  Rais Kikwete akisalimiana na Spika wa Bunge Anne Makinda.




Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda akishiriki misa maalum ya kumbukumbu ya miaka 30 ya kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Hayati Edward Moringe Sokoine iliyofanyika nyumbani kwake Monduli. Kulia kwake ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Mhe. Dkt. Fenera Mkungara, na motto wa Marehemu sokoine Ndugu Joseph Sokoine

Related

OTHER NEWS 405707331113464219

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item