BOKO HARAMU KUWAUZA WASICHANA WALIOTEKWA

Kiongozi wa Boko Haram, Abubakar Shekau Kundi la wapiganaji wa kiislamu nchini Nigeria la Boko Haram limesema linapanga kuwauza was...

Kiongozi wa Boko Haram, Abubakar Shekau

Kundi la wapiganaji wa kiislamu nchini Nigeria la Boko Haram limesema linapanga kuwauza wasichana zaidi ya miambili ambao liliwateka nyara wiki tatu zilizopita.

Hii ni baada ya kundi hilo hatimaye kukiri ndilo lililowateka wasichana hao baada ya kimya cha wiki tatu tangu kutekwa nyara kwao.

Kiongozi wa kundi hilo, Abubakar Shekau alituma kanda ya video ambapo alikiri kwa mara ya kwanza kuwa kundi hilo ndilo liliwateka nyara wasichana hao.

Wasichana hao walitekwa kutoka shule moja iliyo kaskazini mashariki mwa nchi walipokuwa wajinadaa kwa mitihani yao.

Wakati huo huo mwanamke ambaye ni kiongozi wa maandamano ya kushinikiza serikali kuharakisha juhudi zake za kuwaokoa wasichana hao, nchini humo Naomi Mutah aliyekuwa amezuiliwa na polisi kwa amri ya mke wa rais wa nchi hiyo Patience Jonathan ameachiwa huru.

Kumekuwa na shinikizo kwa serikali ya nchi hiyo kwamba haijafanya juhudi kubwa kuwaokoa wasichana hao.

Akizungumza kwa mara ya kwanza kuhusu tukio hilo rais wa Nigeria Goodluk Jonathan amesema kuwa atafanya awezalo kuwakoa wasichana hao.

Takriban watu 1500 wameuawa na kundi hilo mwaka huu likisema kuwa linapigana dhidi ya kile linachosema ni elimu ya kimagharabi.

Related

MBEYA CITY YAAMBULIA PATUPU KWA YANGA, YAFUNGWA 1 - 0

TIMU ya Mbeya City leo imepokea kipigo cha kwanza katika Ligi Kuu ya Bara baada ya kulala kwa bao 1-0 kutoka kwa Yanga kwenye mchezo uliopigwa uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Bao pekee la Y...

TAZAMA PICHA ZA MATUKIO MBALIMBALI YALIYOJILI HUKO MKOANI MBEYA KWENYE MAADHIMISHO YA MIAKA 37 YA CCM

MATEMBEZI YA MSHIKAMANO YALIFANYIKA JIJINI MBEYA Mweneyekiti wa CCM, Rais Jakaya Kikwete akiwasili eneo la Soweto kuongoza  matembezi ya mshikamano ya miaka 37 ya CCM, yaliyofanyika...

RAIS WA ZANZIBAR DKT. SHEIN ALIPOWASILI NCHINI INDIA, TAZAMA PICHA

  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akipokea mashada ya mauwa   wakati wa mapokezi nyake alipowasili katika uwanja wa ndege wa Jaipu...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904763
item