SAGNA ASAJILIWA MANCHESTER CITY KWA MKATABA WA MIAKA MITATU

Beki wa kulia wa Arsenal, Bacary Sagna amekamilisha usajili wake Manchester City kwa kupewa mkataba wa miaka mitatu. Sagna amem...

Beki wa kulia wa Arsenal, Bacary Sagna amekamilisha usajili wake Manchester City kwa kupewa mkataba wa miaka mitatu.

Sagna amemaliza mkataba wake Arsenal, ambapo wakuu wa Emirates walikuwa wakivuta miguu kumpatia mkataba mpya kwa sababu ya umri wake.
Sagna (31) alikuwa kichocheo kikubwa cha mafanikio Arsenal msimu uliomalizika majuzi lakini Arsenal waliona kwamba umri na fedha alizokuwa akidai vilikuwa juu.
Inaelezwa kwamba awali alipewa mkataba wa mwaka mmoja Arsenal akakataa, akapewa wa miaka miwili lakini wakashindwana kwenye malipo, akaamua kuondoka.
Alicheza mechi yake ya mwisho kwenye fainali ya Kombe la Ligi wikiendi iliyopita ambapo Arsenal waliibuka na taji baada ya miaka tisa.
 
Inaelezwa kwamba mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England wamempa mkataba ambao atalipwa pauni 150,000 kwa wiki, ikiwa ni nyongeza kubwa kutoka pauni 80,000 alizokuwa akilipwa Arsenal.
Hata hivyo, Sagna ambaye kocha Arsene Wenger alijaribu kumbakiza, alikuwa akitaka nyongeza hadi pauni 200,000 na miaka mitatu zaidi hapo Emirates, kiwango ambacho kikilinganishwa na umri wake waliona hakikidhi mahitaji.
Sagna alikuwa pia akitakiwa kusajiliwa na klabu nyingine kubwa Ulaya kama Paris Saint Germain,  na Monaco za Ufaransa na  Galatasaray ya Uturuki.
Kutokana na mazingira hayo, Arsenal wameshaanza mazungumzo kwa ajili ya kumsajili Serge Aurier anayecheza Toulouse ya Ufaransa kuziba nafasi ya Sagna.
Aurier anayethaminishwa kwa pauni milioni saba amesema wazi kwamba hawezi kukataa ofa kutoka klabu yoyote ya Ligi Kuu England, hata zilizopanda daraja msimu huu kwa sababu ni ligi kubwa.
Arsenal wameshaanza mazungumzo na klabu yake, ambapo watalazimika kutoa fungu huku Sagna, akiondoka na kusajiliwa bure huko aendako kwa kuwa ni mchezaji huru
 

Related

IGP MANGU AFANYA MABADILIKO YA MAKAMANDA WA POLISI

IGP ERNEST MANGU INSPEKTA Jenerali wa Polisi (IGP) Ernest Mangu, amepangua baadhi ya makamanda wa polisi wa mikoa, wapelelezi na wakuu wa polisi wa usalama barabarani, pamoja na watendaji wen...

NAIBU WAZIRI WA MAJI AMOS MAKALA AONGEA NA WATUMISHI IDARA YA MAJI MOROGORO

 Makala akizungumza jambo katika mkutano huo kutoka kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Maji Halima Mbiru na kulia ni Katibu Tawala Msaidizi Sehemu ya Maji, Esther Lauwo. Baadhi ya wat...

NEC KUTANGAZA TAREHE YA UCHAGUZI JIMBO LA KALENGA

JULIUS MALABA - MKURUGENZI WA UCHAGUZI Dar es Salaam. Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema wiki hii itatangaza tarehe ya uchaguzi mdogo wa ubunge Jimbo la Kalenga, lililopo wazi baada ya ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904746
item