TAARIFA ZA JESHI LA POLISI KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA DODOMA

Kutoka Dodoma Mei 05 majira ya saa saba mchana kulitokea vurugu zilizoanzishwa na wabeba mizigo wa Mji mdogo wa Kibaigwa ambapo taari...


Kutoka Dodoma Mei 05 majira ya saa saba mchana kulitokea vurugu zilizoanzishwa na wabeba mizigo wa Mji mdogo wa Kibaigwa ambapo taarifa inasema zilikua ni vurugu zilizosababisha magari kadhaa kuvunjwa vioo.

Miongoni mwa magari yaliovunjwa vioo ni pamoja na la Mbunge wa Tanga Omary Nundu, gari la Polisi na basi linalofanya safari zake kati ya Dar na Mwanza la Shabaha mbali na kuvunjwa kwa magari hayo pia maduka yaliporwa na hata barabara kuu ya Dodoma-Morogoro ilifungwa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma David Misime amesema Mpaka sasa jeshi la polisi linawashikiliwa watu 34 ambao ni wakazi wa kibaigwa kata ya kibaigwa wilaya ya kongwa kwa makosa ya kufanya fujo na kuharibu mali.

Sehemu nyingine ya taarifa hiyo inasema vijana zaidi ya 300 wakishirikiana na wabeba mizigo wa Kibaigwa walifanya maandamano yasiyo na kibali na kung’oa bango la halmashauri ya kongwa lililokua na tangazo la kukataza wafanyabiashara kuingiza mazao sokoni bila kulipa ushuru.
Baada ya bango hilo vijana hao waliamua kufunga barabara kuu ya Dodoma Morogoro kwa mawe na kuchoma matairi baadae walivamia maduka na kupora vinywaji na kuvunja majokofu.
Chanzo cha vurugu hizo  ni wabeba mizigo wa soko la mazao Kibaigwa  kupinga kitendo cha Halmashauri ya Kongwa kuweka tangazo la kutoza ushuru wa mazao sokoni hapo wakidai kwamba inawakosesha kufanya kazi zao kwani wateja wao wanashindwa kuingiza mazao sokoni.
 

Related

TAMKO LA MH. GODBLESS LEMA

  TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARIJana  majira ya saa nne asubuhi nilipokea taarifa kutoka Chuo cha Uhasibu juu ya tukio la mauaji ya mwanafunzi yaliyotokea jana usiku kwa kuchomwa kisu...

SAKATA LA KOROSHO LIWALE, NYUMBA 20 ZATEKETEZWA

 Takriban nyumba 20 zimeteketezwa katika maandamano yaliyofanywa na wakulima wa Korosho pamoja na waandamanaji wengine Kusini mwa Tanzania. Hii ni kwa mujibu wa mbunge mmoja wa eneo hilo.Mb...

WANAWAKE KWENYE MIEREKA TUPO, HII NI KUTOKA SENEGAL

Nchini Senegal, miereka ya kitamaduni inapendwa zaidi kuliko soka huku wachezaji wakijipatia pesa nyingi na hata kuwa watu maarufu. Katika sehemu nyingi za nchi mchezo huu ni wa wanaume pekee la...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904746
item