TAARIFA ZA JESHI LA POLISI KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA DODOMA

Kutoka Dodoma Mei 05 majira ya saa saba mchana kulitokea vurugu zilizoanzishwa na wabeba mizigo wa Mji mdogo wa Kibaigwa ambapo taari...


Kutoka Dodoma Mei 05 majira ya saa saba mchana kulitokea vurugu zilizoanzishwa na wabeba mizigo wa Mji mdogo wa Kibaigwa ambapo taarifa inasema zilikua ni vurugu zilizosababisha magari kadhaa kuvunjwa vioo.

Miongoni mwa magari yaliovunjwa vioo ni pamoja na la Mbunge wa Tanga Omary Nundu, gari la Polisi na basi linalofanya safari zake kati ya Dar na Mwanza la Shabaha mbali na kuvunjwa kwa magari hayo pia maduka yaliporwa na hata barabara kuu ya Dodoma-Morogoro ilifungwa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma David Misime amesema Mpaka sasa jeshi la polisi linawashikiliwa watu 34 ambao ni wakazi wa kibaigwa kata ya kibaigwa wilaya ya kongwa kwa makosa ya kufanya fujo na kuharibu mali.

Sehemu nyingine ya taarifa hiyo inasema vijana zaidi ya 300 wakishirikiana na wabeba mizigo wa Kibaigwa walifanya maandamano yasiyo na kibali na kung’oa bango la halmashauri ya kongwa lililokua na tangazo la kukataza wafanyabiashara kuingiza mazao sokoni bila kulipa ushuru.
Baada ya bango hilo vijana hao waliamua kufunga barabara kuu ya Dodoma Morogoro kwa mawe na kuchoma matairi baadae walivamia maduka na kupora vinywaji na kuvunja majokofu.
Chanzo cha vurugu hizo  ni wabeba mizigo wa soko la mazao Kibaigwa  kupinga kitendo cha Halmashauri ya Kongwa kuweka tangazo la kutoza ushuru wa mazao sokoni hapo wakidai kwamba inawakosesha kufanya kazi zao kwani wateja wao wanashindwa kuingiza mazao sokoni.
 

Related

MAJAMBAZI WAVAMIA KITUO CHA POLISI KIMANZICHANA NA KUUA ASKARI.

Mnamo 11/06/14 huko kituo kidogo cha Kimanzichana Pwani, watu wasiojulikana waliojifanya kuwa ni raia wema waliingia kituo kidogo cha Polisi Kiman nanzi Chana huku wakikimbia wakiwa na silaha za...

RAIS ATEUA NAIBU MABALOZI

 Bw. Robert Kahendaguza  Bw. Msafiri Marwa UTEUZI WA NAIBU MABALOZI Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete, amefanya uteuzi wa Naibu Mabalozi wawi...

MOTO WATEKETEZA SOKO LA KARUME DAR ES SALAAM

Mabanda ya wamachinga eneo la Soko Karume yameteketea kwa moto usiku wa kuamkia leo, chanzo cha moto huo hakijajulikana. RCP Marieta Minangi amethibitisha kutokea kwa tukio hilo.

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904746
item