TAARIFA ZA JESHI LA POLISI KUHUSU VURUGU ZILIZOTOKEA DODOMA

Kutoka Dodoma Mei 05 majira ya saa saba mchana kulitokea vurugu zilizoanzishwa na wabeba mizigo wa Mji mdogo wa Kibaigwa ambapo taari...


Kutoka Dodoma Mei 05 majira ya saa saba mchana kulitokea vurugu zilizoanzishwa na wabeba mizigo wa Mji mdogo wa Kibaigwa ambapo taarifa inasema zilikua ni vurugu zilizosababisha magari kadhaa kuvunjwa vioo.

Miongoni mwa magari yaliovunjwa vioo ni pamoja na la Mbunge wa Tanga Omary Nundu, gari la Polisi na basi linalofanya safari zake kati ya Dar na Mwanza la Shabaha mbali na kuvunjwa kwa magari hayo pia maduka yaliporwa na hata barabara kuu ya Dodoma-Morogoro ilifungwa.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma David Misime amesema Mpaka sasa jeshi la polisi linawashikiliwa watu 34 ambao ni wakazi wa kibaigwa kata ya kibaigwa wilaya ya kongwa kwa makosa ya kufanya fujo na kuharibu mali.

Sehemu nyingine ya taarifa hiyo inasema vijana zaidi ya 300 wakishirikiana na wabeba mizigo wa Kibaigwa walifanya maandamano yasiyo na kibali na kung’oa bango la halmashauri ya kongwa lililokua na tangazo la kukataza wafanyabiashara kuingiza mazao sokoni bila kulipa ushuru.
Baada ya bango hilo vijana hao waliamua kufunga barabara kuu ya Dodoma Morogoro kwa mawe na kuchoma matairi baadae walivamia maduka na kupora vinywaji na kuvunja majokofu.
Chanzo cha vurugu hizo  ni wabeba mizigo wa soko la mazao Kibaigwa  kupinga kitendo cha Halmashauri ya Kongwa kuweka tangazo la kutoza ushuru wa mazao sokoni hapo wakidai kwamba inawakosesha kufanya kazi zao kwani wateja wao wanashindwa kuingiza mazao sokoni.
 

Related

JAJI WA MAHAKAMA YA RUFANI NCHINI AAPISHWA KUWA JAJI WA MAHAKAMA YA KIMATAIFA YA MAKOSA YA JINAI (ICC)YA NCHINI CAMBODIA

AJI wa Mahakama ya Rufani (T), Mhe.Dr. Stephen Bwana ameapishwa leo (Alhamisi) kuwa Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) ya nchini Cambodia.  Uapisho huo unafuatia baada y...

HIZI NDIZO SILAHA ZA JADI NA CD ZINAZODAIWA KUELEKEZA NAMNA YA KUFANYA MAFUNZO YA KIJESHI KWA MAKUNDI YA AL-SHABAAB NA AL-QAEDA ZILIZOKAMATWA MKOANI MTWARA NA JESHI LA POLISI

CD zilizokamatwa na askari wa jeshi la polisi Mtwara ikiwemo na kuwakamata vijana 11 ambao wanadaiwa walikua wakifanya mazoezi ya kijeshi waliyokua wakijifunza kutoka kwenye CD za magaidi ziliz...

VIONGOZI WA VYAMA VYA UKOMBOZI IHEMI

Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Iringa Ndugu Jesca Msambatavangu akiwaongoza viongozi wa vyama vya ukombozi mara tu walipowasili mkoani Iringa kwa ziara ya siku moja ya kutembelea chuo cha Ihemi, Vion...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item