FRANK LAMPARD KUAGA CHELSEA

 Mchezaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 35 na ambaye ndiye mfungaji bora zaidi wa mabao katika klabu hiyo kwa jumla ya mabao 2...

 Mchezaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 35 na ambaye ndiye mfungaji bora zaidi wa mabao katika klabu hiyo kwa jumla ya mabao 211, anamaliza kandarasi yake mwezi huu.

Tangu alipojiunga na klabu hiyo kutoka West Ham mwaka wa 2001, Lampard ameshinda mataji makuu 11, zikiwemo 3 za ligi ya Premier na ile ya vilabu bingwa mwaka wa 2012.

''Klabu hii imekuwa sehemu ya maisha yangu,” alisema Lampard ambaye anaweza kustaafu ingawa vilabu 16 vinataka kumsajili.

Sasa hivi yuko pamoja na kikosi cha Uingereza mjini Miami kabla ya Kombe la Dunia na hatafanya uamuzi wowote kuhusu hatima yake baada ya mashindano hayo.

Baada ya kusajiliwa kwa Euro milioni 11, Lampard aliichezea Chelsea michuano 688 na kumfanya kuwa mchezaji wa tatu kuwahi kuichezea klabu hiyo mechi nyingi zaidi nyuma ya Ron Harris aliyecheza mechi 795 na Peter Bonetti aliyecheza mechi 729.

Katika muda wake kwenye klabu hiyo iliyoko magharibi mwa London, amewahi pia kushinda mataji 4 ya FA, mawili ya ligi na ligi ya Uropa.

''Nilipojiunga na klabu hii nzuri miaka 13 iliyopita, singewahi kuamini kwamba ningekuwa mwenye bahati ya kucheza mechi nyingi na kushiriki ufanisi namna hii,” aliongezea Lampard, mchezaji bora wa mwaka wa Chelsea mara tatu.

Related

MWANDISHI WA BBC AFARIKI DUNIA GHAFLA.

Mwandishi wa BBC Komla Dumor MWANDISHI wa BBC Komla Dumor amefariki ghafla nyumbani kwake kutokana na mshtuko wa moyo. Alikuwa na miaka 41 alipopata mauti yake.Komla Dumor ameelezewa kuwa mio...

KANUSHO LA Dkt. CHAMI KUHUSIANA NA YALIYO POSTIWA FACEBOOK

Naitwa Cyril August Chami (PhD) Mbunge wa Jimbo la Moshi Vijijini na Mjumbe wa NEC-CCM kupitia Wilaya ya Moshi Vijijini. Nimesikitishwa na kufadhaishwa sana na mtu au watu waliotengeneza akau...

MBATIA ASHINDA NAFASI YA UENYEKITI NCCR MAGEUZI

James Mbatia ameweza kutetea vyema nafasi yake ya Uenyekiti wa chama cha NCCR Mageuzi kwa kupata kura 201 kati ya 227 na  kumpiku mpinzani wake Makofila aliyepata kura 26 kwenye uchaguzi uliof...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item