SUMATRA YATOA UFAFANUZI KUHUSU MALALAMIKO YA CHAKUA

  Rose masaka - MAELEZO DAR ES SALAAM Mamlaka ya  Udhibiti wa Usafirishaji  Majini na  Nchi Kavu (SUMATRA) imetoa ufafanuzi kuwa  ...

 
Rose masaka - MAELEZO DAR ES SALAAM
Mamlaka ya  Udhibiti wa Usafirishaji  Majini na  Nchi Kavu (SUMATRA) imetoa ufafanuzi kuwa  hajafikia muafaka  wa kuwalazimisha abiria wa mikoani kutumia mchakato wa  mbinu  mpya ya ukatishaji wa tiketi  za mabasi ya kwenda mikoani kwa njia ya mtandao  ikiwemo wa simu za mkononi kwa kuwa baadhi ya wamiliki wa mabasi wamegawanyika, na bado haukidhi mahitaji ya sasa.
 
Kauli hiyo imetolewa leo na Meneja wa Mawasiliano wa SUMATRA, David Mziray wakati akizungumza na mwandishi wa habari wa Idara ya Habari(MAELEZO) baada ya Chama Cha Kutetea  Abiria Tanzania(CHAKUA) kuilalamikia, SUMATRA ndio inayochelewesha mchakato huo na wameairisha kufanyika kikao cha wadau kilichotakiwa kufanyika Mei30,mwaka huu.
Malalamiko hayo  yalitolewa na Mwenyekiti wa CHAKUA, Hassan Mchanjama, alipokuwa akiongea na katika mkutano na waandishi wa habari,uliofanyika leo kwenye ukumbi wa Idara  ya Habari(MAELEZO).
 
Aidha kutokana na malalamiko hayo, Mziray alisema ni kweli kikao hicho, kiliairishwa kutokana na sababu zisizoweza kuzuilika huku akisisitiza kikao hicho kilikuwa cha mashauriano na si cha kutoa uamuzi. 
Mziray aliongeza kwamba , hata hivyo  baadhi ya wamiliki wa mabasi hayo, wamegawanyika kwani wapo wanaouunga mkono utaratibu huo na  wengine wanaupinga kutokana kwamba watakosa abiria , upatikanaji wa fedha unachukua muda mrefu na mapato yao yatajulikana.
“Hatuwezi kuulazimisha utaratibu huo utumike kwa sasa kwa sababu nilizotaja na pia  kuna baadhi ya  wananchi  hawatumii simu za mkononi,” alisema Mziray.
Mziray alisema waliishauri CHAKUA  watoe elimu kwa wamiliki hao ili kuwezesha  utaraibu huo utumike kwa wale wanauunga mkono na wanaoweza kuutumia, bali kwa abiria ambao ni vigumu kutumia utaratibu wa zamani utumike.
 
 CHAKUA iimetoa  malalamiko hayo kwa  mamlaka hiyo  baada ya kuwasilisha mchakato huo kwa kumwandikia  barua , Waziri wa Uchukuzi  Dkt. Harrison Mwakyembe , ambapo  uongozi wa chama hicho  ulidai kuwa  aliiagiza SUMATRA  kuitisha kikao  na wadau .
Kikao hicho   kiliitishwa Desemba 17,mwaka huu ,ambapo wadau hao ambao ni Wamiliki wa Mabasi(TABOA), CHAKUA  na Jeshi la Polisi la Usalama Barabarani walikubaliana kuanzishwa kwa mchakato huo kwa  kukiitisha kikao na wadau baada ya miezi mitatu.
 
Aidha Mchanjama amesema kuwa utaratibu waliougundua ni mzuri na wenye manufaa kwa wamiliki , abiria na Serikali  kwani itarahisisha muda wa kukata tiketi bila kwenda kituo cha mabasi.
Ameongeza kwa kusema kuwa nauli zitakuwa ni halali na zilizoainishwa na SUMATRA ili kuondoa kero kwa abiria ya kuongezewa nauli hususani siku za sikukuu au shule zikifunguliwa au kufungwa.
 
“Utaratibu huu unarisisha abiria kudai fidia pindi anapopata madhara katika mabasi kama ajali ,kupotelewa na mzigo na magari kugoma” alisema Mchanjama.
 
Aliongeza  kuwa kila kitu kitakuwa wazi katika mtandao, hivyo ni rahisi kwa abiria kupata nyaraka za basi husika pindi anapopata tatizo,pia mmiliki atafaidika kwa kupata mapato moja kwa moja tofauti na sasa pesa zinapita mikononi mwa watu wengi.
 
Kuna taasisi nyingi za serikali na watu binafsi ambazo zimekuwa mfano mzuri katika utumiaji wa mtandao ambazo ni TRA,TANESCO,DAWASCO na Benki mbalimbali.

Related

OTHER NEWS 3452305917090014230

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item