MAALIM SEIF AHUDHURIA MKUTANO WA KIMATAIFA WA UCHUMI

  Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif, akisalimiana na Kiongozi wa Istambuli wakati akiwasili katika ukumbi wa mkuta...

 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif, akisalimiana na Kiongozi wa Istambuli wakati akiwasili katika ukumbi wa mkutano. wa Kimataifa wa Uchumi unaofanyika nchini huo.
 Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif akiwasili ukumbi wa mkutano na Ujumbe wake.

      Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Maalim Seif akiwa na Mkutano na Ujumbe wake




Na Khamis Haji, Istanbul
                          
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Maalim Seif Sharif Hamad amewasili nchini Uturuki akiongoza ujumbe wa Zanzibar katika mkutano wa Kimataifa wa Uchumi ulioanza leo jijini Istanbul.

Katika mkutano huo uliolenga kuweka mikakati ya matumizi bora ya rasilimali kwa maendeleo ya kiuchumi, zaidi ya wajumbe 500 kutoka mataifa tafauti, wakiwemo wanasiasa, wafanyabiashara, wataalamu wa uchumi na fedha na wawakilishi wa sekta binafsi wanahudhuria.

Akizungumza katika kikao cha utangulizi kabla ya kufunguliwa rasmi mkutano huo, Mkurugenzi wa Mashirika ya Kimataifa na Serikali wa Mkutano wa Kiuchumi wa Dunia (WEC), Carl Bjorkman ameyahimiza mataifa kutoa kipaumbele katika kuimaarisha miundo mbinu ya kiuchumi kama njia muhimu ya kuwapatia fursa za kimaendeleo wananchi wao.

Mkurugenzi huyo amesema mataifa mengi bado hayaoneshi mafanikio makubwa katika ukuaji wa uchumi, huku sekta nyingi zinazogusa maendeleo ya watu wao zikiyumba, hali ambayo inapaswa kudhibitiwa kwa mataifa kuwa na mikakati ya pamoja ya kukuza maendeleo ya kiuchumi.

Amesema miongoni mwa matatizo makubwa kwa nchi nyingi ni kukosekana fursa za kiuchumi zinazoweza kuzaa ajira nyingi kwa wananchi, hali inayochangia kukosekana imani ya wananchi na baadaye kuathiri utulivu na amani ambao ni msingi wa ukuaji wa uchumi na maendeleo.

“Tukiungana mataifa ya Ulaya, Asia, America na Afrika tukiweza kuzitumia rasilimali tulizonazo katika maeneo yetu kwa kuzingatia vipaumbele vya ukuaji wa uchumi, tutaweza kuleta mabadiliko na kuunda fursa nyingi kwa wananchi katika Mabara yote”, amesema Bjorkman.

Mkurugenzi huyo amehimiza utaratibu wa mataifa kuchagua maeneo machache yenye ufanisi kushirikiana kwa mujibu wa mazingira yao, ambapo mataifa yataweza kushirikiana katika kuyaendeleza, badala ya kuweka vipaumbele vingi kwa wakati mmoja, hali ambayo haileti mafanikio makubwa katika utekelezaji wake.

Ujumbe wa Zanzibar pia unawashirikisha Waziri wa Biashara, Viwanda na Masoko, Nassor Ahmed Mazrui, Katibu wa Tume ya Mipango, Amina Khamis Shaaban na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Uwekezaji Vitega uchumi (ZIPA), Salum Nassor

Related

KIFAHAMU KIKOSI CHA TIMU YA TAIFA YA NIGERIA KITAKACHO SHIRIKI FAINALI ZA KOMBE LA DUNIA 2014

 Kocha wa timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya Nigeria, Steohen Keshi ametaja kikosi cha wachezaji 23 kitakochoshiriki fainali za kombe la dunia ( Fifa World Cup 2014) zinazotarajiwa kuanza ju...

TASA KUSHIKA MIMBA KUPITIA SAYANSI

Wengi miongoni mwa wanawake wanapoolewa ndoto yao kubwa huwa ni kupata watoto. Ndoto hiyo inaposhindwa kutimia kwa njia ya kawaida, basi juhudi zaidi hufanyika . Mbinu mpya ya kisayansi ambayo...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904982

HOT POSTSRECENTArchive

RECENT

Archive

item