MCHUNGAJI CHRISTOPHER MTIKILA KUMBURUZA MAHAKAMNI MGOMBEA URAIS CHADEMA EDWARD LOWASSA NA MWENZAKE WA CCM KWA KUIINGIZIA SERIKALI HASARA..

Alisema wagombea hao kwa nyakati tofauti, wameshiriki kuiingizia Serikali hasara ya mabilioni ya fedha ambapo wanasheria wa chama hic...



Alisema wagombea hao kwa nyakati tofauti, wameshiriki kuiingizia Serikali hasara ya mabilioni ya fedha ambapo wanasheria wa chama hicho wapo katika hatua za mwisho ili wafunguliwe mashtaka mahakamani. 

Mchungaji Mtikila aliyasema hayo Dar es Salaam jana, alipozungumza na waandishi wa habari akisisitiza kuwa, wagombea hao wamepoteza sifa za kuwania nafasi hiyo akidai hawana vigezo kwa mujibu wa sheria. 


Aliongeza kuwa, Bw. Lowassa, anahusishwa na sakata la kampuni ya Kufua Umeme ya Richmond na kuishangaa CHADEMA akidai chama hicho kilipata umaarufu wa kupinga vitendo vya ufisadi lakini wamempokea Bw. Lowassa ana tuhuma kama hiyo. 


"Kipindi cha nyuma, CHADEMA walianzisha operesheni nyingi 
ikiwemo ya Sangara na Movement for Change zikiwa na lengo la kupinga ufisadi, kwanini wamempokea Lowassa waliyemuita fisadi. 


"Hii ina maana kuwa, ndani ya CHADEMA hakuna siasa, nawapongeza baadhi ya viongozi wa chama hicho na wanachama wao ambao kimsingi hawakubaliani na matakwa ya viongozi wa juu," alisema.


Akimzungumzia Dkt. Magufuli, alimhusisha na tuhuma ya uuzwaji wa nyumba za Serikali akidai kitendo hicho kimeisababishia hasara Serikali lakini hakupelekwa mahakamani kwa kutumia madaraka yake vibaya kama ilivyokuwa kwa Basil Mramba, Daniel Yona ambao hivi sasa wanatumikia kifungo gerezani. 


Alisema nyumba hizo zilikuwa makazi ya viongozi kama Majaji, Makatibu Wakuu na Watendaji waandamizi serikalini ambao wengi wao walilazimika kuishi hotelini kwa gharama za Serikali.


MAJIRA

Related

MATOKEO YA UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI ULIOFANYIKA 09/02/2014 KATIKA KATA MBALIMBALI NCHINI, CCM YASHINDA KWA KISHINDO KATA 23, CHADEMA WAAMBULIA KATA 3 NA NCCR YAPATA KATA 1

MATOKEO YA JUMLA NDIYO YALIVYOLIPOTIWA KUTOKA VYANZO MBALIMBALI VYA UDIWANI.CCM YAPATA KATA 24 HUKU CHADEMA IKIPATA KATA 3MATOKEO YA UDIWANI KATA YA SOMBETINI ARUSHA. CHADEMA KURA 2548CCM...

MBUNGE AUAWA JAMHURI YA AFRIKA YA KATI

Mbunge mmoja wa Jamuhuri ya Afrika ya Kati, ambaye alikuwa katika mstari wa mbele kupinga mauaji ya Waislamu nchini humo, ameuawa kwa kupigwa risasi katika mji mkuu wa nchi hiyo Bangui. Jean-Em...

RAIS KIKWETE AHUTUBUA MKUTANO WA BARAZA LA VYAMA VYA SIASA

Rais Jakaya Mrisho Kikwete akitoa hotuba yake kwenye ufunguzi wa mkutano wa Baraza la Vyama vya Siasa leo Februari 6, 2014 katika Ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es salaam. ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904812
item