HII NDIO RATIBA KAMILI YA RAIS BARACK OBAMA ILIYOTOLEWA NA WIZARA YA MAMBO YA NDANI NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA

Rais wa Marekani, Mhe. Barack Obama anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 01 Julai, 2013 mchana kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili. Katika Uwan...


Rais wa Marekani, Mhe. Barack Obama anatarajiwa kuwasili nchini tarehe 01 Julai, 2013 mchana kwa ziara ya kitaifa ya siku mbili.

Katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam, Mhe. Rais Obama ambaye atafuatana na Mkewe Mama Michelle atapokelewa na Mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete.

Baada ya mapokezi, Mhe. Rais Obama atakwenda Ikulu kwa mazungumzo rasmi na Mhe. Rais Kikwete. Aidha, atafanya mkutano na Wafanyabiashara na kuhudhuria Dhifa ya Kitaifa.

Tarehe 2 Julai 2013, Mhe. Rais Obama atatembelea Mitambo ya kufua Umeme ya Symbion iliyopo Ubungo, Dar es Salaam na kuzindua rasmi Mpango Maalum wa Maendeleo ya Nishati Barani Afrika ulioanzishwa na Marekani (Power Africa Initiative).

Mpango huo utaanza na nchi saba ambazo ni: - Tanzania, Kenya, Uganda, Ethiopia, Ghana, Nigeria na Sudan Kusini.

Mhe. Rais Obama anatarajiwa kuondoka nchini tarehe 02 Julai 2013.


IMETOLEWA NA:
 WIZARA YA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA KIMATAIFA, 
DAR ES SALAAM
30 JUNI, 2013 0 MAONI

Related

WAZIRI MKUU WA LIBYA AACHIWA HURU BAADA YA KUTEKWA LEO ALFAJIRI

Waziri mkuu wa Libya, Ali Zeidan akiwa amezungukwa na watu eneo lisilojulikana Waziri mkuu wa Libya, Ali Zeidan ameripoti kuachiwa huru baada ya kutekwa leo alfajiri. Tukio hilo lilitokea majira y...

BOTI YAWAKA MOTO

Wavuvi wapatao 11 wameokolewa kutoka kwenye jahazi iliyokuwa ikiwaka moto kwenye bahari ya hindi, 10km toka bandari ya Dar es salaam lei asubuhi. Chanzo cha ajali hiyo ni injini, polisi imethibitish...

JAJI WA MAHAKAMA YA RUFANI NCHINI AAPISHWA KUWA JAJI WA MAHAKAMA YA KIMATAIFA YA MAKOSA YA JINAI (ICC)YA NCHINI CAMBODIA

AJI wa Mahakama ya Rufani (T), Mhe.Dr. Stephen Bwana ameapishwa leo (Alhamisi) kuwa Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) ya nchini Cambodia.  Uapisho huo unafuatia baada y...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item