IFAHAMU METHADONE-TIBA TEGEMEZI KWA WATUMIA DAWA ZA KULEVYA

  Methadone ni dawa inayotumika kutibu utegemezi wa dawa zingine za kulevya mfano; heroin,codeine,pethine na morphine. Dawa ...

 
Methadone ni dawa inayotumika kutibu utegemezi wa dawa zingine za kulevya mfano; heroin,codeine,pethine na morphine.
Dawa hii hutolewa kwa kipimo maalum chini ya usimamizi wa mtaalamu.Hivyo hupunguza maambukizi ya VVU na Homa ya Ini [B na C] kwa wanaojiunga.Hapa Tanzania,kwa sasa huduma hii inatolewa na hospitali ya Taifa Muhimbili.
Tiba ya methadone huzuia ‘arosto’ na kupunguza au kuondoa utegemezi wa dawa za kulevya.
 
Je,Methadone huleta utegemezi?
Jibu:Hapana.
Kwanza kabisa matumizi ya methadone hutolewa kama tiba na kupewa kwa wale wenye utegemezi wa dawa za kulevya.
Kwa wagonjwa wa namna hii kwao ni mbadala salama wa dawa za kulevya wanazotumia kama vile heroin.
Inawaweka huru kutoka kwenye kulazimika kutafuta dawa za kulevya na kuwapa fursa ya kuboresha maisha yao.

Je,utajisikiaje ukitumia methadone?
Watu wakianza kutumia tiba ya methadone,baadhi hujisikia raha iliyozidi na kujisikia kusinzia hali ambayo pia huletwa na baadhi ya dawa nyingine za kulevya.
Je,unaweza kutumia methadone na dawa zingine?
Methadone ni dawa yenye nguvu sana na inaweza kuwa na mwingiliano na dawa nyingine na kuleta madhara.
Mweleze daktari au mfamasia kuhusu dawa ulizo kunywa kabla ya kutumia methadone.
Ni muhimu kumweleza mfamasia au daktari kama umekunywa pombe au dawa ya usingizi kwa mfano valium,fenegani au piriton maana huweza kuleta kifo kama itanywewa pamoja na Methadone.
Kuchanganya dawa ya methadone na dawa nyingine za kulevya kunaweza kusababisha mwili kuzidiwa na dawa(overdose),hali ambayo inaweza kuhatarisha maisha.

Related

TUJUZANE 310182253294103666

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item