MAAZIMIO YA KIKAO CHA BARAZA KUU LA UONGOZI LA TAIFA CUF KILICHOFANYIKA DAR ES SALAAM TAREHE 21-22 AGOSTI, 2013

Baraza Kuu la Uongozi Taifa la The Civic United Front (CUF- Chama Cha Wananchi) limekutana na kufanya kikao chake cha kawaida kwa muj...

Baraza Kuu la Uongozi Taifa la The Civic United Front (CUF- Chama Cha Wananchi) limekutana na kufanya kikao chake cha kawaida kwa mujibu wa katiba ya chama, kikao ambacho kimeongozwa na Mwenyekiti wa Chama Taifa, Mhe. Prof Ibrahim Lipumba. Kikao hicho kimefanyika katika ukumbi wa Shaaban Mloo, Dar es salaam, tarehe 21-22 Agosti, 2013. Katika kikao hicho, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa lilipokea, kuzijadili na kuzifanyia maamuzi agenda mbalimbali zilizowasilishwa na Kamati ya Utendaji ya Taifa ikiwa ni pamoja na;
  1. Taarifa ya utekelezaji wa kazi za chama Mei-Julai, 2013.
  2. Taarifa ya utekelezaji wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.
  3. Taarifa ya utekelezaji wa kazi za wabunge na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuanzia Januari-Julai, 2013.
  4. Taarifa ya kutekwa na kuteswa kwa viongozi wa CUF na JWTZ mkoani Mtwara.
  5. Program ya kuimarisha Chama Sept 2013-Julai 2014 na Uchaguzi wa ndani ya Chama. 
  6. Hali ya kisiasa, kiuchumi na kijamii nchini, pamoja na masuala mengineyo yaliyojadiliwa na kufanyiwa maamuzi.

Baada ya mjadala wa kina kuhusiana na agenda hizo, Baraza Kuu la Uongozi la Taifa limefikia maazimio yafuatayo;

1. Kuhusu Taarifa ya Kazi za Chama kwa Kipindi cha Mei-Julai, 2013;
Baraza Kuu limepokea taarifa ya kazi za Chama kwa kipindi cha mwezi Mei-Julai, 2013 na kuipongeza Kamati ya Utendaji Taifa kwa kazi iliyofanywa katika kipindi hicho, ikiwa ni pamoja na kuipongeza kwa kufanikishan ushindi na kulirejesha Jimbo la Chambani, Mkoa wa Kusini Pemba kwa kukipatia chama chetu ushindi wa kutosha. Pia Baraza linawapongeza Wapiga Kura wa Wadi ya Ng’omeni katika Jimbo la Mkoani, Wialya ya Mkoani kwa ushindi iliofanyika Miezi Michache iliopita. CUF inawashukuru wananchi wote wa Chambani na Wadi ya Ng’omeni na kuwaahidi utumishi wa dhati kwa maendeleo yao na taifa kwa ujumla.

Baraza Kuu limeiagiza Kamati ya Utendaji ya Taifa kufanya utafiti wa kina juu ya matokeo yasioridhisha ya uchaguzi mdogo wa marudio katika kata 26 uliofanyika nchini na kuleta mapendekezo ya utekelezaji katika kikao kijacho cha Baraza kwa ajili ya kufanyiwa kazi.

2. Taarifa ya Utekelezaji Kazi za Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar.
Baraza kuu la uongozi la Taifa linawapongeza Mawaziri na Manaibu Mawaziri kwa kusimamia majukumu yao vizuri na kuweza kudhihirisha wazi kuwa CUF na viongozi wake wanauwezo mkubwa wa kuwaletea mabadiliko ya maisha Wazanzibari. CUF inawaomba Wanzanzibari wote kutuunga mkono katika jitihada hizi za kuleta mabadiliko ya kisiasa na kiuchumi kwa wananchi wote.

3. Taarifa ya Utekelezaji wa kazi za Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kuanzia Januari-Julai,2013

Baraza kuu limepokea taarifa ya utekelezaji wa kazi za Wabunge na Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi kwa kipindi cha Januari-Julai, 2013.
Linawapongeza kwa kazi nzuri ya kuzisimamia serikali zote mbili kikamilifu na kuweza kufichua ubadhilifu na ufisadi wa kutisha katika wizara mbalimbali.

Baraza Kuu linahitaji Kamati za Bunge na Mkaguzi na Mdhibiti wa hesabu za Serikali kufanya ukaguzi wa kina na kutoa maelezo kwa Watanzania na hususani Wananchi wa Mtwara kwamba fedha iliyotengwa kwenye bajeti ya mwaka 2010/2011, Sh. 540 milioni ambazo zilikuwa ziende kwenye mradi wa Mnazi Bay Gas and Electricity Development Project, fedha hiyo imetumikaje wakati mradi wenyewe haupo, na hali mradi huo ulikuwa umeingizwa katika vitabu vya bajeti ya Serikali.

Wawaeleze Watanzania ni kwa sababu gani mradi huo wameufuta na fedha hizi zimekwenda wapi? Baraza Kuu pia limetaka upembuzi yakinifu wa mradi wa bomba la gesi na mikataba ya kujenga bomba iwekwe wazi ili wananchi waweze kubaini faida na hasara zake.

Aidha, limewataka Wabunge kufuatilia taarifa ya ufisadi zilizofichuliwa na kamati ya hesabu za serikali kuu kiasi cha shilingi bilioni 247 za commodity import support hazijalipwa Hazina na kuhakikisha wahusika wanawajibishwa. Vilevile Bunge lichukue hatua za kuwawajibisha Mawaziri waliolidanganya Bunge kuhusu miradi hewa ya barabara iliyotengewa fedha shilingi bilioni 252.

4. Hali ya amani, usalama wa Taifa na Haki za Binaadamu Nchini;

a) Kuhusu Kuteswa na Kudhalilishwa kwa Naibu Mkurugenzi wa Oganaizesheni Shaweji Mketo na wenzake.Baraza Kuu la Uongozi linalaani vikali vitendo vya kikatili walivyofanyiwa Viongozi wa Cuf na JWTZ vya kuwateka nyara, kuwatesa na kuwadhalilisha katika kambi ya JWTZ, Naliendele, Mtwara. Aidha, linalaani vikali hatua za Jeshi la Polisi, Mtwara la kuwabambikizia kesi ya uchochezi Mketo na wenzake hali wakijua fika kuwa askari wa JWTZ waliwateka nyara na kuwatesa kinyume sheria.

Kuteswa na kudhalilishwa kwa Mketo na wenzake kunatokana na kauli ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda, aliotamka Bungeni ya Piga tu, Tumechoka. Wakati Mketona wenzake wanateswa, askari wa JWTZ walieleza kuwa wamepewa ruhusa ya kupiga hata kuua wakorofi wachache na hawatachukuliwa hatua zozote. Hatima utekelezaji wa kauli hiyo unaendelea katika maeneo mbali mbali ya Nchi kama vile Mtwara na Handeni Kata ya Misima.

b) Madawa ya kulevya
Baraza Kuu linasikitishwa na kukithiri kwa biashara ya madawa ya kulevya, huku Vyombo vya Dola vikijikita zaidi katika kushughulikia Viongozi wa Dini, Vyama vya Siasa na Wananchi kadhaa katika maeneo mbali mbali na kwa kutumia Nguvu kubwa na rasilimali nyingi zaidi ili kutia khofu wananchi wasiweze kuhoji na kuisimamia Serikali ya CCM kwa ahadi walizotoa kwa Watanzania.

Baraza Kuu linasikitishwa na kuona kuna mapungufu makubwa kwa Jeshi la Polisi kupitia Kitengo cha Kuzuia Madawa ya Kulevya kilichopo Uwanja wa Ndege wa Dar es Salaam mpaka kufikia Waziri wa Uchukuzi Dr Harison Mwakyembe kushughulikia jambo hilo.

Related

OTHER NEWS 7445705858924300952

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item