PINDA KWENDA KITETO KUTAFUTA SULUHU YA MAPIGANO

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda leo anakwenda Wilaya ya Kiteto, Arusha kutafuta suluhu ya mapigano baina ya wakulima na wafugaji katika Hif...

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda leo anakwenda Wilaya ya Kiteto, Arusha kutafuta suluhu ya mapigano baina ya wakulima na wafugaji katika Hifadhi ya Embroi Murtangosi yaliyosababisha vifo vya watu 10.
Mwandishi wa Habari wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Irene Bwire alisema jana: “Ni kweli Waziri Mkuu atakwenda kutembelea wilayani Kiteto ili kuongoza juhudi za kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.”

Polisi waanzisha msako
Maofisa wa Polisi kutoka Makao Makuu ya jeshi hilo wanaongoza operesheni ya kuwasaka wahusika wa mapigano hayo kwa kutumia helikopta.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Manyara, Akili Mpwapwa alisema msako huo unaongozwa na Kamishna wa Operesheni wa Polisi, Simon Sirro... “Operesheni inaendelea porini lakini hadi sasa hatujakamata mtu. Mapigano yanayoendelea Kiteto ni ya kuviziana.”
Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Martha Umbulla amezitaka pande zote kuacha vita na kuwataka waliovamia ardhi ya Kiteto kuondoka kwa hiari.
Chadema waibana Serikali
Waziri Kivuli wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Rose Kamili ameitaka Serikali kuchukua hatua za haraka kumaliza mgogoro huo.
Katika taarifa yake aliyoitoa jana, Kamili alisema licha ya Bunge kuunda kamati kwa ajili ya kuchunguza migogoro ya wakulima na wafugaji nchi nzima, hali bado ni tete katika eneo hilo.
Alisema Serikali inatakiwa kujitafakari juu ya uwezo wake wa kushughulikia matatizo ya haraka, badala ya kuwa mabingwa wa kushughulika na matokeo ya tatizo.

Mgogoro
Mgogoro huo ulioanza mwaka 2006, unatokana na wafugaji na wakulima kugombea ardhi kwenye eneo la Hifadhi ya Embroi Murtangosi.
Mapigano kati ya pande hizo mbili yamesababisha watu wanaokadiriwa kufikia 30 kuuawa.
Hifadhi hiyo yenye hekta 135,000, ina vyanzo vingi ya maji na madini ya aina ya chumvi, haitakiwi kuguswa kwa shughuli za kilimo wala ufugaji.
Wafugaji wanashinikiza utekelezaji wa amri ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania, ambayo mwaka 2009 iliwaamuru wakulima kuondoka katika eneo hilo.
Mwaka 2006, wakulima waliishtaki Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto katika Mahakama ya Wilaya na kushinda kesi.
Halmashauri ilikata rufaa Mahakama Kuu lakini wakulima waliibuka washindi tena. Ilikata rufaa Mahakama ya Rufani ambako ilishinda na wakulima walitakiwa kuondoka.
MWANANCHI

Related

RIPOTI YA CAG KUZIGUZA CHADEMA, CCM

Dar es Salaam.  Bunge la Bajeti linaanza vikao vyake mjini Dodoma na moja ya kazi zake zitakazovuta hisia za wengi ni Ripoti ya Mwaka 2012/13 ya Mashirika ya Umma na Taasisi za Serikali it...

MENEJA WA BARCLAYS MBARONI KWA WIZI WA FEDHA, NI BAADA YA KUPANGA TUKIO LA KIUJAMBAZI NDANI YA BENKI HIYO JIJINI DAR ES SALAAM.

Dar es Salaam.  Hatimaye Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam limetoa taarifa ya wizi uliotokea katika Benki ya Barclays, Tawi la Kinondoni Aprili 15, mwaka huu, likisema tukio hi...

BASI LA A.M COACH LAPATA AJALI ENEO LA IPULI NA KUSABASHA KIFO CHA MWANAFUNZI MMOJA

 Umati mkubwa wa watu ambao ulifiika kushuhudia ajali hiyo mbaya  Maafisa wa Chama cha Msalaba Mwekundu mkoa wa Tabora walifika eneo la tukio na kusaidia majeruhi wa ajali hiyo. ...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item