TAARIFA KUHUSU KIKAO CHA KAMATI KUU CHA CHADEMA KESHO

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa ka...

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa kauli ifuatayo;
Ni kweli kutakuwa na mkutano maalum wa Kamati Kuu ya chama kesho tarehe 3 Januari 2014 Jijini Dar Es Salaam. Ajenda kuu katika mkutano huo ni tatu;

Mosi: Kupokea taarifa kuhusu mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba.
Kamati Kuu itapokea taarifa juu ya kupitishwa kwa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba 2013, kupitishwa kwa muswada wa kura ya maoni wa 2013, uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum na kutolewa kwa Rasimu ya Katiba Mpya.

Pili: Kupokea utetezi (wa mdomo) wa wanachama watatu kuhusu tuhuma mbalimbali zilizoelekezwa kwao.
Wanachama hao walishajulishwa makosa yao kwa maandishi na wamewasilisha utetezi wao wa maandishi. Wataitwa kwenye kikao kwa kuzingatia matakwa ya kanuni 6.5.2 (b) na 6.5.2 (d) kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.

Tatu: Mpango Kazi wa Chama kwa mwaka 2014
Mpango Kazi wa chama ni sehemu ya hatua za utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Chama wenye dhima ya kuleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya chama na taifa.

John Mnyika
Mkurugenzi wa Mawasiliano

Related

BOTI YAWAKA MOTO

Wavuvi wapatao 11 wameokolewa kutoka kwenye jahazi iliyokuwa ikiwaka moto kwenye bahari ya hindi, 10km toka bandari ya Dar es salaam lei asubuhi. Chanzo cha ajali hiyo ni injini, polisi imethibitish...

JAJI WA MAHAKAMA YA RUFANI NCHINI AAPISHWA KUWA JAJI WA MAHAKAMA YA KIMATAIFA YA MAKOSA YA JINAI (ICC)YA NCHINI CAMBODIA

AJI wa Mahakama ya Rufani (T), Mhe.Dr. Stephen Bwana ameapishwa leo (Alhamisi) kuwa Jaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Makosa ya Jinai (ICC) ya nchini Cambodia.  Uapisho huo unafuatia baada y...

HIZI NDIZO SILAHA ZA JADI NA CD ZINAZODAIWA KUELEKEZA NAMNA YA KUFANYA MAFUNZO YA KIJESHI KWA MAKUNDI YA AL-SHABAAB NA AL-QAEDA ZILIZOKAMATWA MKOANI MTWARA NA JESHI LA POLISI

CD zilizokamatwa na askari wa jeshi la polisi Mtwara ikiwemo na kuwakamata vijana 11 ambao wanadaiwa walikua wakifanya mazoezi ya kijeshi waliyokua wakijifunza kutoka kwenye CD za magaidi ziliz...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item