TAARIFA KUHUSU KIKAO CHA KAMATI KUU CHA CHADEMA KESHO

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa ka...

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa kauli ifuatayo;
Ni kweli kutakuwa na mkutano maalum wa Kamati Kuu ya chama kesho tarehe 3 Januari 2014 Jijini Dar Es Salaam. Ajenda kuu katika mkutano huo ni tatu;

Mosi: Kupokea taarifa kuhusu mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba.
Kamati Kuu itapokea taarifa juu ya kupitishwa kwa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba 2013, kupitishwa kwa muswada wa kura ya maoni wa 2013, uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum na kutolewa kwa Rasimu ya Katiba Mpya.

Pili: Kupokea utetezi (wa mdomo) wa wanachama watatu kuhusu tuhuma mbalimbali zilizoelekezwa kwao.
Wanachama hao walishajulishwa makosa yao kwa maandishi na wamewasilisha utetezi wao wa maandishi. Wataitwa kwenye kikao kwa kuzingatia matakwa ya kanuni 6.5.2 (b) na 6.5.2 (d) kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.

Tatu: Mpango Kazi wa Chama kwa mwaka 2014
Mpango Kazi wa chama ni sehemu ya hatua za utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Chama wenye dhima ya kuleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya chama na taifa.

John Mnyika
Mkurugenzi wa Mawasiliano

Related

JOYCE KIRIA WA WANAWAKE LIVE AMTAFUTA MUMEWE!!!

MTANGAZAJI WA KIPINDI CHA TV WANWAK LIVE JOYCE KIRIA, NDANI YA KITUA CHA EATV AKIWA AMESHIKILIA WATOTO WAKE LINCORN & LINGATONE, WAKATI ALIPOZUMNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI NJE YA JENGO LA IDAR...

WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA ITALIA BERLUSCON AHUKUMIWA KIFUNGO CHA MIAKA 7 JELA

Waziri mkuu wa zamani wa Italia Silvio Berlusconi kushoto na kulia ni Karima El MahrougITALY:Jopo la majaji limemuhukumu waziri mkuu wa zamani Silvio Berlusconi kifungo cha miaka saba (7) jela kwa kos...

OFISI YA CCM WILAYA YA MBINGA YACHOMWA MOTO

Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake ambao hawapo pichani. Katibu wa chama cha Mapinduzi wilaya ya Mbinga Anastasia Amasi ak...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904763
item