TAARIFA KUHUSU KIKAO CHA KAMATI KUU CHA CHADEMA KESHO

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa ka...

Kutokana na maswali kutoka kwa wanahabari wa vyumba mbalimbali vya habari juu ya agenda za kikao cha Kamati Kuu kesho, Chama kimetoa kauli ifuatayo;
Ni kweli kutakuwa na mkutano maalum wa Kamati Kuu ya chama kesho tarehe 3 Januari 2014 Jijini Dar Es Salaam. Ajenda kuu katika mkutano huo ni tatu;

Mosi: Kupokea taarifa kuhusu mchakato na maudhui ya mabadiliko ya katiba.
Kamati Kuu itapokea taarifa juu ya kupitishwa kwa marekebisho ya sheria ya mabadiliko ya katiba 2013, kupitishwa kwa muswada wa kura ya maoni wa 2013, uteuzi wa wajumbe wa Bunge Maalum na kutolewa kwa Rasimu ya Katiba Mpya.

Pili: Kupokea utetezi (wa mdomo) wa wanachama watatu kuhusu tuhuma mbalimbali zilizoelekezwa kwao.
Wanachama hao walishajulishwa makosa yao kwa maandishi na wamewasilisha utetezi wao wa maandishi. Wataitwa kwenye kikao kwa kuzingatia matakwa ya kanuni 6.5.2 (b) na 6.5.2 (d) kupewa nafasi ya kujitetea mbele ya kikao kinachohusika.

Tatu: Mpango Kazi wa Chama kwa mwaka 2014
Mpango Kazi wa chama ni sehemu ya hatua za utekelezaji wa Mpango Mkakati wa Chama wenye dhima ya kuleta uongozi bora, sera sahihi, mikakati makini na oganizesheni thabiti kwa maendeleo endelevu ya chama na taifa.

John Mnyika
Mkurugenzi wa Mawasiliano

Related

MBUNGE ROSE KAMILI: MWENYEKITI WA CCM ALIHUSIKA KUNITEKA

  Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Rose Kamili, aliyedai ametekwa na kuteswa wakati wa uchaguzi mdogo mkoani Iringa, amemtuhumu Mwenyekiti wa CCM mkoani humo, Jessica Msambatavangu kuwa ana...

WABUNGE SASA KUANZA KUPITIA RASIMU YA KATIBA

Wajumbe wa Bunge Maalum la Katiba. Bunge Maalumu la Katiba linaendelea na kikao chake na miongoni mwa shughuli zinazotarajiwa kufanywa  kuanzia leo, ni kurekebisha baadhi ya kanuni z...

BIG RESULT NOW YAKUSANYA MABILIONI KATIKA KIPINDI CHA NUSU MWAKA

Msemaji Mkuu wa Wizara ya Fedha, Ingiahedi Mduma, akizungumza wakati wa Semina maalum kwa wanahabari, iliyofanyika katika Hoteli ya Kilimanjaro Park, Misugusugu Kibaha, leo Machi 28, 2014. Sem...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item