TAPELI WA KIKE ALIYETAPELI KWA NJIA YA AIRTEL MANOY AFUNGWA KIFUNGO NZEGA MKOANI TABORA, AWATAPELI MAWAKALA FEDHA KWA NJIA YA MTANDAO.

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Nzega mkoani Tabora, imemhukumu mkazi wa hapa kwenda jela miezi sita, kwa kosa la utapeli wa fedh...


MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Wilaya ya Nzega mkoani Tabora, imemhukumu mkazi wa hapa kwenda jela miezi sita, kwa kosa la utapeli wa fedha kwa njia ya mtandao wa Airtel Money kwa mawakala mbalimbali wilayani humo.
Akitoa hukumu hiyo, Hakim Mkazi Mfawidhi, Joseph Ngomelo, alisema mshitakiwa Helena Alexandria, atakwenda jela miezi sita baada ya kukiri kufanya utapeli huo.

Mshitakiwa huyo alikiri kutapeli mawakala mbalimbali wa Airtel Money waliopo Nzega mjini kwa njia ya mtandao na kujipatia fedha kwa njia isiyo halali.

Alisema kifungo cha mama huyo kitakuwa fundisho kwa wanawake wangine wenye tamaa, kwani makosa kama hayo yakiachiwa yanaweza kuleta madhara makubwa kwa jamii.

Awali Mwendesha Mashitaka wa Polisi Mkaguzi Msaidizi, Melito Ukongoji, aliiambia Mahakama hiyo kuwa Januari mosi mwaka 2014, mshitakiwa ambaye ni mkazi wa Nzega mjini, aliiba kwa kutumia mtandao wa Kampuni ya Airtel Money.

Alidai kuwa Hellena alikuwa akitumia ujumbe mfupi wa maneno wenye muamala wa kutoa pesa Sh 40,000 Airtel Money na kujipatia Sh 40,000 kwa kila wakala kwa nyakati tofauti.

Akijitetea, mshitakiwa alikiri kuhusika na tuhuma hizo kwa nyakati tofauti na kuongeza kuwa lengo lilikuwa ni kutafuta fedha za kujikimu kimaisha kutokana ugumu wa maisha.

Kabla ya kutoa hukumu hiyo Mwendesha Mashitaka aliiomba Mahakama hiyo itoe adhabu kwa mshitakiwa huyo ili iwe fundisho kwa watu wenye tabia kama hizo za wizi wa utapeli kwa njia ya mtandao.
HABARI LEO

Related

TCRA YAZIFUNGULIA REDIO IMAAN YA MOROGORO NA KWA NEEMA YA MWANZA

Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) leo imezifumgulia Redio Imaan ya Morogoro na Kwa Neema inayorusha matangazo yake kutoka jijini Mwanza, zilizokuwa zimefungiwa kwa muda wa miezi 6 kutokana na sababu z...

KIKAO CHA BUNGE LA AFRIKA MASHARIKI CHASHINDWA KUFANYIKA

Mbunge Peter Mathuki kutoka Kenya aliyewasilisha hoja binafsi kwenye bunge la EAC jana   Sakata la vikao vya Bunge la Afrika Mashariki kufanyika kwenye nchi wanachama kwa mzunguko limeingi...

SERIKALI HAIWEZI KUTAJA MAJINA YA VIGOGO WA BIASHARA YA MADAWA YA KULEVYA, WABUNGE WAMO KATIKA ORODHA HIYO

DODOMA.  WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi amesema baadhi ya majina ya wabunge yametajwa miongoni mwa watu wanaoshukiwa kujihusisha na biashara ya...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904769
item