MAJAMBAZI YAUA POLISI DAR ES SALAAM (SAMAHANI KWA PICHA)

   Mwili wa askari aliyeuawa ukiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Temeke   Mwili wa jambazi mwingine ukiwa...

   Mwili wa askari aliyeuawa ukiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Temeke


 Mwili wa jambazi mwingine ukiwa umeharibika vibaya baada ya kipigo kikali kutoka kwa wananchi wenye hasira.
 Mwili wa askari polisi ukiwa umepakiwa kwenye gari ya polisi tayari kupelekwa hospitali ya Temeke kuhifadhiwa.

Askari polisi mmoja wa kituo cha polisi Chang'ombe, Mkoa wa kipolisi wa Temeke, ameuawa kikatili siku ya ijumaa mchana baada ya kupigwa risasi ya kifua na majambazi waliokuwa wanajaribu kutoroka baada ya kufanya tukio la kihalifu. Askari hao waliokuwa doria katika eneo la Wailes walijikuta wakishambuliwa kwa risasi na majambazi hao mara baada ya majambazi hao kujaribu kukimbia katika eneo la tukio kwa kutumia usafiri wa pikipiki kipindi ambapo askari polisi walikuwa karibu na eneo la tukio. Hata hivyo wakati askari hao wakijaribu kuwafukuza majambazi hao wawili kwa lengo la kuwakamata ndipo jambazi mmoja alitoa bastola na kumpiga risasi ya kifua askari huyo na kufariki pale pale.

Hata hivyo katika harakati za kujaribu kukimbia majambazi hao walianguka na pikipiki waliyokuwa wakitumia ndipo wakaamua kutimua mbio mitaani na kuingia katika nyumba moja ambapo walijificha na kujifanya kama ni wakazi wa eneo hilo, baada ya wnanchi na polisi kufika katika nyumba hiyo, baadhi ya majirani waliwaambia polisi kwamba wameona watu hao wameingia katika nyumba hiyo. Baada ya polisi kuingia waliwakuta watu hao wakiwa wametulia kama kwamba wao ni wakaazi wa nyumba hiyo na wala hawajui lililotokea.

Baada ya kuwatambua watu hao, polisi waliwatia nguvuni huku wananchi wenye ghadhabu waking'ang'ania kuwa wanataka kuwaua sababu wameshaua askari mmoja. Baada ya vuta nikuvute kati ya wananchi na askari hao ambao walikuwa wachache, wananchi walifanikiwa kuwachukua majambazi hao kwa nguvu kutoka mikononi mwa polisi na kuanza kuwapiga kwa silaha mbalimbali za kienyeji yakiwemo mawe na marungu mpaka watuhumiwa hao wakapoteza maisha.
 
Source: Matukio Blog

Related

MFANYA BIASHARA ARUSHA AMWAGIWA TINDIKALI

Mfanyabiashara Japhet Minja amelazwa katika Hospitali ya Arusha Lutheran Centre (Seliani) jijini Arusha, baada ya kumwagiwa kimiminika kinachosadikiwa kuwa tindikali usoni na watu wasiojuli...

WAZIRI MKUU WA LIBYA AACHIWA HURU BAADA YA KUTEKWA LEO ALFAJIRI

Waziri mkuu wa Libya, Ali Zeidan akiwa amezungukwa na watu eneo lisilojulikana Waziri mkuu wa Libya, Ali Zeidan ameripoti kuachiwa huru baada ya kutekwa leo alfajiri. Tukio hilo lilitokea majira y...

BOTI YAWAKA MOTO

Wavuvi wapatao 11 wameokolewa kutoka kwenye jahazi iliyokuwa ikiwaka moto kwenye bahari ya hindi, 10km toka bandari ya Dar es salaam lei asubuhi. Chanzo cha ajali hiyo ni injini, polisi imethibitish...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904754
item