UDAHILI CHUO CHA HABARI ZANZIBAR KUANZA JUNE 2

Chuo cha Uandishi wa Habari Zanzibar kinawatangazia Wanafunzi wote waliomba kujiunga na chuo kwa mwaka wa masomo 2014/2015 kwenda kuch...

Chuo cha Uandishi wa Habari Zanzibar kinawatangazia Wanafunzi wote waliomba kujiunga na chuo kwa mwaka wa masomo 2014/2015 kwenda kuchukua barua za udahili (admission letter) chuoni hapo kuanzia Jumatatu ya tarehe 2, June 2014.

 Aidha chuo kinawajulisha vijana wote waliomaliza kidato cha nne na cha sita pamoja na wafanyakazi wa Taasisi za umma na binafsi, kuwa bado zipo nafasi chache za kujiunga na...
masomo katika Ngazi ya Stashahada (Diploma in Journalism), Ngazi ya Cheti (Certificate in Journalism) na Cheti cha Muda mfupi (Short Course in Journalism). Kwa wale watakaojiunga na course za muda mrefu watasoma lugha ya kichina, kingereza na kiswahili bure.
 
Pia Chuo cha Uandishi wa Habari Zanzibar kinatoa Mafunzo ya Programu Maalum ya Muda Mfupi katika masuala ya Uhusiano kwa umma, Utayarishaji Vipindi vya Redio na TV, Upigaji Picha za aina zote na Uandishi pamoja na lugha ya Kichina.
Kwa maelezo zaidi fika Chuoni Vuga Mkabala na Afisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi au wasiliana nasi kwa simu Na. 077-424 877, 0778-415789 au 0718 – 307 193.
 
Kwa walioko Pemba fomu zinapatikana Ofisi kuu ya Wizara ya Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo au wasiliana na Wakala wetu kwa simu Na. 0777 870191.
 
Jiunge sasa na taaluma ya uandishi wa Habari kwa kupitia Chuo cha Uandishi wa Habari Zanzibar kilichosajiliwa na NACTE na kutambulika kimataifa.

Related

ELIMU 8704604948656298128

Post a Comment

emo-but-icon

FOLLOW US

.

LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

RECENT

Archive

item