SIKU YA MABAHARIA 2014 YAADHIMISHWA

Kila mwaka ifikapo tarehe 25 Juni, Jumuiya ya Kimataifa inaadhimisha Siku ya Mabaharia Duniani. Hawa ni watu wanaofanya kazi kwa muda ...

Kila mwaka ifikapo tarehe 25 Juni, Jumuiya ya Kimataifa inaadhimisha Siku ya Mabaharia Duniani. Hawa ni watu wanaofanya kazi kwa muda mrefu katika kipindi chote cha mwaka, ili kuhakikisha kwamba, mizigo wanayoshughulikia bandarini inawafikia walengwa kwa wakati muafaka. Hii ni sehemu ya ujumbe kutoka kwa Bwana Koji Sekimizu, wakati huu wa maadhimisho wa Siku ya Mabaharia Duniani.
 
 Kuna Meli ambazo zimesheheni mizigo kutoka sehemu mbali mbali za dunia zinazohitaji kupakuliwa kwa ajili ya walaji wa Ulaya. Ni mazao ya wakulima kutoka mashambani, madini na malighafi kwa ajili ya matumizi ya viwanda. Hizi ni meli zinazobeba nishati ya mafuta na bidhaa zake kwa ajili ya matumizi mbali mbali ya binadamu. Shughuli zote hizi zinazalisha pato kwa ajili ya ustawi na maendeleo ya mabillioni ya watu duniani.

Lakini inasikitisha kuona kwamba, Mabaharia wapatao millioni 1. 5 wanakabiliwa na hali ngumu ya maisha kila siku, lakini hawa ndio injini ya uzalishaji na ukuaji wa uchumi kimataifa. Ni watu wanaoishi na kukabiliana na hatari kwa kufanya kazi katika mazingira magumu na hatarishi, katika hali mbali mbali za hewa, ni kundi ambalo linapata fursa kiduchu ya kukutana na kuchanganyikana na watu wengine katika Jamii. Kazi ni ngumu inayohitaji uwajibikaji makini.

Mabaharia wanajikuta kwamba, kwa muda mrefu wanatengana na familia zao; wanatishiwa maisha kutokana na vitendo vya kiharamia vinavyofanywa huko Baharini. Siku ya Mabaharia Duniani ni mwaliko kwa wananchi sehemu mbali mbali za dunia kuonesha mshikamano na Mabaharia pamoja na kuwapongeza kwa kazi kubwa wanayoifanya kwa ajili ya kusukuma mbele gurudumu la maendeleo na uchumi wa dunia.

Bwana Koji Sekimizu anasema, Maadhimisho ya Siku ya Mabaharia kwa Mwaka 2013 yalipata mafanikio makubwa kwani vyombo vingi vya mawasiliano ya jamii, vilishiriki katika kuunga mkono kampeni ya maadhimisho ya siku hii. Hata mwaka huu, watu wanahamasishwa kushiriki katika kampeni ya kuunga mkono juhudi za maboresho ya maisha ya Mabaharia sehemu mbali mbali za dunia. Hawa ni watu ambao wamewaonjesha mamillioni ya watu huduma mbali mbali kwa njia ya bidhaa zinazotumika, kumbe kuna haja ya kusema, asanteni Mabaharia.


Related

Never Underestimate Your Partner’s Work

A man came home from work and found his 3 children outside, still in their pyjamas, playing in the mud, with empty food boxes and wrappers strewn around garden.  The door of his wife’s ...

A Must Read: This is Sad! Women Don’t Ever Be Too Desperate To Get Things In Life

Katika pitapita zangu za kusoma  mtandaoni nimekutana na hii story ya mwanamama aliyekuwa desperate kupata mtoto, mwisho wa siku akakutana na mengine. Isome na wewe ujifunze kitu kutoka kwake, e...

81st Wedding Anniversary: Longest Married Couple Shares Secrets Of Their Happy Marriage

John & Ann Betar on their wedding day John and Ann Betar eloped on Nov. 25, 1932, fleeing their close-knit Syrian neighborhood in Bridgeport, Connecticut, and driving as fast as they coul...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904819
item