HITIMISHO LA SHINDANO LA ELIMU YA UWEKEZAJI KWA WANAZUONI (DSE SCHOLAR INVESTMENT CHALLENGE) KUFANYIKA AGOSTI 13 2014

Soko la Hisa Dar es Salaam (Dar es Salaam Stock Exchange), kwa udhamini wa benki ya NMB, Selcom na FSDT, linapenda kuwajulisha wana...


Soko la Hisa Dar es Salaam (Dar es Salaam Stock Exchange), kwa udhamini wa benki ya NMB, Selcom na FSDT, linapenda kuwajulisha wanafunzi wa elimu ya juu nchini walioshiriki katika shindano la elimu ya uwekezaji kwa mwaka 2014 (DSE Scholar Investment Challenge 2014) kuwa maandalizi yote ya kuhitimisha shindano hili kwa sasa yamekamilika.

Mchakato wa kutambua nafasi ya kila mshiriki wa shindano umemalizika. Majina ya wanafunzi 50 wanaoongoza katika shindano hilo yamebandikwa katika mtandao wa DSE (www.dse.co.tz) kwenye kipengele cha Investment Challenge.

Sherehe za kuwatambua washindi na kuwapatia vyeti na zawadi zitafanyika tarehe 13 August 2014 jijini Dar es Salaam. Mialiko ya kuhudhuria sherehe hizo inaendelea kutumwa kwa njia ya simu.
 
Shindano la elimu ya uwekezaji kwa wanazuoni (DSE Scholar Investment Challenge) lilianza tarehe 01/04/2014 na kumalizika tarehe 30/06/2014. Wanafunzi washiriki walipewa nafasi ya kutumia simu zao za mkononi ili kununua na kuuza hisa zinazouzwa katika soko la hisa (DSE) la Dar es Salaam. Kila mshiriki alipewa mtaji (virtual capital) wa shilingi milioni moja. Ushiriki kwa shindano hili ulikuwa ni bure na huru kwa yeyote aliyependa.

Nia kubwa ya shindano hili ni kuwapatia vijana walio katika vyuo vya elimu ya juu nchini fursa ya kuwekeza katika soko la hisa kwa majaribio na kuangalia mitaji yao ikikua. Elimu hii pia ni muhimu katika kujenga utamaduni wa utunzaji fedha na uwekezaji miongoni mwa vijana walio vyuoni (ambao ni viongozi, wawekezaji, wahasibu, wachumi, na washauri watarajiwa).

Washiriki walitegemewa kushindana kukuza mitaji waliyopewa kwa kipindi cha miezi mitatu. Mafanikio ya shindano na elimu hii ni makubwa sana. Mwanafunzi anayeongoza amekuza mtaji wake kutoka shilingi milioni moja aliyopewa na kufikisha shilingi milioni nne (kwa kipindi cha miezi mitatu tu).
 
DSE inawapongeza zaidi ya wanafunzi 5,000 walioshiriki katika shindano na elimu hii muhimu kwao na taifa kwa ujumla.
Shindano na elimu hii imepangwa kufanyika tena mwakani na kuwahusisha wanafunzi wengi zaidi ya elfu tano walioshiriki mwaka huu. DSE imepanga kuwawezesha wanafunzi na vijana nchini kutumia simu pamoja na intaneti mwakani ili kuwapa uwanja mpana zaidi wa kushiriki. Mipango ya baadaye ni kuwashirikisha wanafunzi walioko kwenye shule za sekondari pia.
 
 

Related

TAARIFA MAALUM KUTOKA BARAZA LA MITIHANI TANZANIA.

Normal 0 false false false EN-US X-NONE X-NONE MicrosoftInternetExplorer4 ...

GARI LAUA WANAFUNZI MTWARA

Gari ndogo imevamia mchakamchaka wa wa wanafunzi wa shule ya masingi Sabodo, Mtwara alfajiri ya leo nakuua  wanafunzi wanne (4). Wanafunzi 21 wapo hoi hospitalini na wengine 26 wameruhusiwa, ...

KIDATO CHA KWANZA 2014 KUDAHILIWA KIELEKTRONIKI

Profesa Eustella Bhalalusesa WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, kuanzia mwaka huu imeanza kutumia mfumo wa kielektroniki kwa wanafunzi wanaoingia kidato cha kwanza. Imeelezwa kuwa utarat...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904916
item