SABA MBARONI KWA MAUAJI YA WANAWAKE MKOANI ARUSHA

Na Joseph Ngilisho, Arusha JESHI la Polisi Mkoani hapa linawashililiwa watu saba,wanaotuhumiwa kujihusisha na matukio ya mauaji na un...


Na Joseph Ngilisho, Arusha
JESHI la Polisi Mkoani hapa linawashililiwa watu saba,wanaotuhumiwa kujihusisha na matukio ya mauaji na unyang’anyi wa kutumia silaha n'a kuwapiga risasi wanawake.

Akizungumza na waandishi wa habari mkoani hapa, Kamanda wa jeshi hilo, Liberatus Sabas,aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Japhet Lomnyak (25) mkazi wa Sakina,Nehemia Kweka (34) wa Ngaramtoni, Adam Mussa (30) wa Majengo, Tito Loomoni (25) wa Shamsi, Joseph  Loomoni (29) wa Shamsi, Abdallah Magilani (22) mkazi wa Oldadai na Emmanuel Magilani (23) mkazi wa Oldadai.

Alisema watuhumiwa hao wamehusika katika tukio la Agosti 21 mwaka huu, maeneo ya Olasiti ambapo walkiwa na pikipiki aina ya Toyo, walimjeruhi kwa risasi Christen Nickson mkazi wa Olasiti.

Alisema watuhumiwa walifukuza gari aina ya Corolla na baada ya kusimama walimuamuru dereva ambae ni baba wa marehemu wapatie fedha na kupatiwa shilingi 2,000 huku akiwambia fedha nyengine ziko kwenye gari.

Alisema wakati dereva huyo alipoingia garini huku watuhumiwa wakimsubiri ateremke awapatie fedha, aliondoa gari kwa ghafla na majambazi hayo kufyatua risasi zilizomuua mtoto huyo.





Tukio jengine ni la mauaji ya Shamimu Rashidi Yulu (30) yaliyofanyika Agosti 6 mwaka huu majira ya saa 3:30 usiku katika maeneo ya Kwa Iddi ambapo mama huyo alikuwa akielekea nyumbani kwake.


Alipiogwa risasi shingoni na kufariki dunia akiwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Seliani.

Related

MDEE: JIANDIKISHENI KATIKA DAFTARI KUEPUSHA WIZI WA KURA

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee Wakati miezi tisa ikiwa imebaki Tanzania kufanya uchaguzi mkuu, Watanzania wametakiwa kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura ...

AUA MKE KWA RUNGU AKITUHUMU KUCHEPUKA

Kamanda wa polisi wa mkoa, Kamishina Msaidizi, ACP. Thobias Sedoyeka akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake (hawapo pichani). SINGIDA. WATU wawili wamekufa mkoani Singida katik...

AJIFUNGUA PACHA WA KIKE WALIOUNGANA SEHEMU YA KIFUA, TUMBO

   MUSOMA. Mwanamke mmoja mkazi wa Kata ya Buhare, Manispaa ya Musoma mkoani Mara, Helena Paulo (20), amejifungua watoto pacha wa kike walioungana eneo la kifuani hadi tumboni wakiw...

Post a Comment

emo-but-icon
:noprob:
:smile:
:shy:
:trope:
:sneered:
:happy:
:escort:
:rapt:
:love:
:heart:
:angry:
:hate:
:sad:
:sigh:
:disappointed:
:cry:
:fear:
:surprise:
:unbelieve:
:shit:
:like:
:dislike:
:clap:
:cuff:
:fist:
:ok:
:file:
:link:
:place:
:contact:


LISTEN / DOWNLOAD MUSIC HERE:

Total Pageviews

904758
item